Rais Samia afanya uteuzi…

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema kuwa Nyamanga anachukua nafasi ya Esmaily Rumatila ambaye ameteiliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Edward Nyamanga kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (OMR) upande wa Mazingira.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema kuwa Nyamanga anachukua nafasi ya Esmaily Rumatila ambaye ameteiliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Taarifa hiyo imesema “Nyamanga anachukua nafasi ya Esmaily Hassan Rumatila ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)”

Nyamanga ataapishwa leo Jumatatu Januari 10, 2022 Ikulu ya Chamwino Dodoma.