Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

RC Kagaigai ataka ushirikiano Kilimanjaro

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai akizungumza mara baada ya kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa mkuu wa Mkoa huo, Anna Mghwira.Picha na Janeth Joseph

Muktasari:

  • Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amewataka wakuu wa wilaya, watendaji wa halmashauri pamoja na wakuu wa idara kufanya kazi  kama timu ili kuleta ufanisi.

Moshi. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amewataka wakuu wa wilaya, watendaji wa halmashauri pamoja na wakuu wa idara kufanya kazi  kama timu ili kuleta ufanisi.

Kagaigai ameyasema hayo leo Jumanne Mei 25, 2021 katika makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Anna Mghwira.

Amewataka wananchi kumpa ushirikiano wa kutosha ili aweze kutekeleza yanayokusudiwa na Serikali.

“Rais amenileta huku nimsaidie kutekeleza ilani ya CCM katika kuwatumikia wananchi, ninapenda kufanya kazi kama timu, ofisi yangu kila siku itakuwa wazi ili mtu yeyote mwenye shida na matatizo nimwone na nimsikilize tuone namna ya kutatua changamoto zake.”

“Nawaomba sana wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri pamoja na watendaji wote wanisaidie kwa maana ya kuacha ofisi zao wazi ili waweze kuwapokea wananchi na kusikiliza kero zao na kuzitatua. Huu Mkoa nataka tuutendee haki, ni mkoa wetu sote kwa hiyo sitawaangusha wananchi nawaahidi kuwatumikia,” amesema.