Serengeti Festival ni bandika bandua mpaka asubuhi

New Content Item (1)
Serengeti Festival ni bandika bandua mpaka asubuhi

Muktasari:

Tamasha la Serengeti Festival limeanza leo Jumamosi Desemba 26,  2020 katika viwanja vya Uhuru, Dar es Salaam.

Dar es Salaam. Tamasha la Serengeti Festival limeanza leo Jumamosi Desemba 26,  2020 katika viwanja vya Uhuru, Dar es Salaam.

Tamasha hilo linahusisha wasanii zaidi ya  60 ambao  watatumbuiza jukwaa moja,  wakiwemo  wasanii wa muziki wa kizazi kipya waliotamba miaka ya nyuma,  vikundi vya ngoma za asili, sarakasi na michezo ya kuigiza.

New Content Item (1)
Serengeti Festival ni bandika bandua mpaka asubuhi

Katika ufunguzi jukwaa la Serengeti Festival lilishambuliwa na kikundi cha ngoma za asili cha Disciples Flow Choir ambalo lilitumia dakika 25 kutoa burudani.

Ofisa sanaa mwandamizi wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata),  Abel Ndaga ameieleza  Mwananchi Digital kuwa, vikundi 13 vya ngoma vitatumbuiza mpaka saa 1 jioni  kisha wasanii wa muziki wa kizazi kipya watapewa nafasi.

New Content Item (1)
New Content Item (1)

"Vikundi vitatumbuiza mpaka saa moja, kisha Bongofleva ndo itaanza na msanii wa kwanza kupanda atakuwa Nini. Kimsingi watatumbuiza mpaka asubuhi, " amesema.

New Content Item (1)
Serengeti Festival ni bandika bandua mpaka asubuhi

Tamasha hilo litafanyika kwa siku mbili katika mikoa miwili tofauti. Leo ni Dar ea Salaam na kesho Desemba 27 itakuwa zamu ya wakazi wa Bagamoyo mkoani Pwani.

Wilayani Bagamoyo tamasha hilo  litafanyika katika viwanja vya Tasuba.

Imeandikwa na Kelvin Kagambo