Serikali yatangaza mapumziko siku ya Sensa

Muktasari:

Tanzania itafanya Sensa ya Watu na Makazi Agosti 23, 2022

Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia Agosti 23, 2022 kuwa siku ya mapumziko.

 Lengo ni kuwezesha Watanzania kushiriki Sensa ya Watu na Makazi. Awali ilitangazwa kuwa siku hiyo haitakuwa aya mapumziko.

Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa iliyotolewa leo Alhamisi Agosti 18, 2022 kupitia akaunti yake ya Twitter imesema, Rais Samia ameridhia siku hiyo iwe ya mapumziko.

“Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameridhia tarehe 23 Agosti 2022 iwe siku ya mapumziko ili Watanzania wawepo majumbani na waweze kuwapokea makarani wa sensa na kutoa maelezo sahihi,” amesema Msigwa