Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Vijana wapewa mafunzo ya ujasiriamali

Muktasari:

  • Vijana waishio katika mazingira magumu wilayani hapa, wamepewa mafunzo maalumu ya uanzishaji miradi ya kiuchumi itakayowawezesha kuendesha maisha yao na kusaidia familia zao.

  

Mufindi. Vijana waishio katika mazingira magumu wilayani hapa, wamepewa mafunzo maalumu ya uanzishaji miradi ya kiuchumi itakayowawezesha kuendesha maisha yao na kusaidia familia zao.

Mafunzo hayo  yanayojumuisha kata tatu za Igoda , Luhunga  na Mdabulo  kutoka wilaya ya Mufindi  mkoani Iringa yanatolewa kwa kushirikisha vijana hao ambao baadhi yao ni waliokatisha masomo kwa changamoto za maisha wakiwamo mabinti waliopata ujauzito.

Akizungumza Mkufunzi wa mafunzo hayo, John Kalolo kutoka  shirika lisilo la kiserikali la RLABS –Tanzania, amesema  kuwa  mafunzo hayo ni maalum kwa ajili ya  kuwajengea  uwezo  wa katika ujasiliamali.

"Maeneo mengi ya vijijini kuna fursa  nyingi za kufanya ambazo kimsingi  ni moja kati ya  mtaji mkubwa kwa mtu ambae  anatamani  kuwa mjasiliamali hivyo iwapo  wahusika wataondokana na fikra mgando  za kutegemea fedha  wanaweza kupiga hatua katika maisha," amesema Kalolo. 

Amesema ili vijana hao waondokane na dhana potofu, ni lazima wajitambue kabla ya kuanza shughuli ya ujasilimali na baada ya hapo wanaweza kuomba mikopo ya kuboresha ujasiliamali.

Kalolo amesema ujasiliamali wa ususi kwa wasichana ni kazi ambayo anaweza kuanza kwa ubunifu usio tegemea fedha na ndipo wanaweza kuboresha kwa kutafuta eneo litakalohitaji fedha za kuboresha zaidi.

Kwa upande wake meneja  wa mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM), Zilipa Mgeni amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha vijana zaidi ya 770 wakiwemo  watoto  150 yatima kupata mbinu za kujiajiri.

Amesema mradi  huo wa YAM ni wa miaka minne toka mwaka 2021/2024 umefadhiliwa na Serikali  ya Finland  chini ya taasisi yake ya Diaconess kwa  ushirikiano  wa  Serikali ya Tanzania chini ya Halmashauri ya  wilaya  ya Mufindi na taasisi ya  Foxes Community and Wild Life Conservation.