Arsenal ilivyokwaa kisiki Ligi Kuu England
Muktasari:
- Arsenal inabaki kileleni lakini tofauti yao na wapinzani wao wa karibu imepungua
Licha ya Arsenal kuonekana karibu na ushindi wa 11 mfululizo katika Ligi Kuu ya England, wenyeji Sunderland walionyesha ari ya kupambana hadi mwisho wakitimiza kauli yao mashuhuri iliyoandikwa kwenye kuta za uwanja wao: “’Til The End” (hadi mwisho).
Bao la Brobbey lilitokana na mpira wa kichwa uliopigwa na Dan Ballard, na likapokelewa kwa shangwe kubwa si tu katika mji wa Wearside, bali pia kwenye kambi za wapinzani wa Arsenal kama Liverpool na Manchester City, ambao walifurahia matokeo hayo yaliyowaweka karibu na kilele cha ligi.
Arteta alionekana mwenye huzuni baada ya mchezo, akitoka uwanjani akifananishwa hisia zake na mtu aliyeporwa pochi yake, kwa jinsi alivyopokonywa matokeo sekunde za mwisho.
Bao la kwanza la mchezo lilifungwa na Ballard ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa akademi ya Arsenal.
Alipachika shuti kali lililomshinda kipa David Raya, na akashangilia bila kujizuia, licha ya historia yake na The Gunners.
Arsenal, iliyokuwa imepata clean sheet nane mfululizo kabla ya mchezo huu, ilijibu kwa mabao mawili kipindi cha pili kupitia Bukayo Saka na Leandro Trossard.
Bao la Trossard lilikuwa la kuvutia, akipiga shuti kali lililokwenda moja kwa moja hadi kona ya juu ya goli, lakini hata hivyo halikutosha kuzuia Sanderland kusawazisha matokeo katika dakika za majeruhi.
Mashabiki wa nyumbani walionyesha hamasa kubwa, kila mpira wa kuokolewa ukishangiliwa kana kwamba ni bao, hali iliyoongeza presha kwa Arsenal.
Kama alivyoeleza Le Bris baada ya mchezo:
“Tulilazimika kutoa somo la kujituma. Wachezaji wangu wako tayari kupigana hadi tone la mwisho la jasho. Na tukafanikiwa, tena kwa mara nyingine.”
Kwa matokeo haya, Arsenal inabaki kileleni lakini tofauti yao na wapinzani wao wa karibu imepungua, huku Arteta akikiri kuwa sare hiyo ni somo kwamba hakuna mchezo rahisi katika Ligi Kuu.
Sunderland, kwa upande wao, wameonyesha kuwa si wageni katika ligi hiyo, bali ni timu yenye ari mpya ya kupambana hadi mwisho.