Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mchumba wa Ronaldo atoa picha yake na kichanga mtandaoni

Muktasari:

Nyota huyo sasa ni baba wa watoto wanne baada ya mchumba wake Georgina Rodriguez kujifungua hivi karibuni

Madrid, Hispania. Siku chache baada ya kujifungua mtoto wa kike, mchumba wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez ametuma picha katika mtandao kijamii akiwa amemshika kichanga chake.

Katika picha hiyo aliweka ujumbe mzito, Rodriguez aliwashukuru madaktari na wauguzi wa hospitali kwa huduma mzuri waliyompa na kujifungua salama.

 "Kuwa mama na kuanza malezi ya mtoto wangu ni jambo linalonifanya nijisikie mtu mwenye furaha isiyokuwa na kifani," aliandika katika ukurasa wake wa Instagram.

"Sasa amepatikana  mtoto Alana Martina wote tunafuraha isiyokuwa na kifani.

"Nataka kutoa shukrani zangu kwa wahudumu wote kwa ungalizi mzuri waliotupatia kabla, wakati na baada ya kujifungua.

"Pia, tunawashukuru marafiki, ndugu na watu wote waliotupigia simu na kututumia ujumbe na wengine kuja kututembelea hapa."