Yanga, Simba mguu sawa, CAF yapuliza kipyenga
Muktasari:
- Mashindano ya CAFTanzania itawakilishwa na Yanga na Simba katika Ligi ya Mabingwa Afrika huku Azam na Singida Black Stars zikiwakilisha katika Kombe la Shirikisho.
Dar es Salaam. Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetangaza rasmi kalenda ya mechi za msimu wa 2026/27 wa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika mashindano hayo Tanzania itawakilishwa na Yanga na Simba katika Ligi ya Mabingwa Afrika huku Azam na Singida Black Stars zikiwakilisha katika Kombe la Shirikisho.
Msimu uliopita klabu hizo ziliweka rekodi kwa zote nne kuvuka kucheza hatua ya makundi ya mashindano hayo, lakini zilishindwa kufuzu kwa hatua robo fainali.
Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, msimu wa 2026/27 utaanza kwa hatua ya kwanza ya mchujo, ambapo mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa kati ya Septemba 4 hadi 6, 2026, huku marudi-ano yakifanyika Septemba 11 hadi Septemba 13 mwaka huu.
Hatua ya pili ya mchujo itaanza kwa mechi za mkondo wa kwanza kati ya Oktoba 16 na Oktoba 18 maaka huu na mechi za marudiano zitachewa Oktoba 23 hadi 25, 2026.
Baada ya hatua za mchujo kukamilika, hatua ya makundi ya mashindano yote mawili itaanza mwishoni mwa mwezi Novemba 2026.
Ratiba ya hatua za mchujo
Hatua ya kwanza (Mkondo wa kwanza), Septemba 4–6 2026
Hatua ya kwanza (Marudiano) Septemba 11 hadi 13, 2026
Hatua ya pili (Mkondo wa kwanza) Oktoba 16– Oktoba 18, 2026
Hatua ya pili (Marudiano), Oktoba 23–25, 2026
Ratiba ya hatua ya makundi
Mzunguko wa kwanza ni Novemba 27–29, 2026
Mzunguko wa Pili ni Desemba 4–6, 2026
Mzunguko wa tatu, Desemba 18–20, 2026
Mzunguko wa nne ni Januari 8–10, 2027
Mzunguko wa tano ni Januari 15–17, 2027
Mzunguko wa sita ni Januari 22–24, 2027
Ratiba ya hatua za mtoano
Robo fainali (Mkondo wa kwanza), Februari 26–28, 2027
Robo fainali (Marudiano), Machi 5–7, 2027
Nusu fainali (Mkondo wa kwanza), Aprili 9–11, 2027
Nusu fainali (Marudiano), Aprj 16–18, 2027
Fainali itachezwa kati ya Mei Mei na 31, 2027, kulingana na ratiba itakayothibitishwa na CAF baadaye.