Siku kadhaa baada ya kutokea kifo cha pacha Alif Athuman Ally na Khalifa Athuman Ally ambao walidaiwa kunyweshwa sumu maeneo ya Yombo Vituka jijini Dar es salaam, kaka wa marehemu hao Alli Athuman Dilunga amesema familia imesikitishwa na kitendo hicho huku wakivitaka vyombo vya haki kutoa adhabu aliyehusika na tukio hilo.