Wakati matumizi ya mate yakiwa maarufu kwa wengi wakati wa kujamiiana, hasa yanapotumika kama aina fulani ya kilainishi hasa ukeni na hivyo kuleta ladha ya tendo, habari si njema sana kwa watumiaji wa mate hayo wanapoburudika, hasa kwa wanandoa.

Wataalamu wa afya wamesema kuna ongezeko la magonjwa yanayosababishwa na maambukizi ya fangasi na bakteria katika via vya uzazi vya mwanamke, huku chanzo kikubwa kikitajwa kuwa ni mate.