‘Profesa Lipumba’ mpya kupatikana leo CUF

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Muktasari:

Wajumbe zaidi ya 700 wa Mkutano Mkuu wa dharura wa CUF wanakutana mjini Dar es Salaam leo kumchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Ibrahim Lipumba aliyejiuzulu wadhifa huo mwaka jana.

Dar es Salaam. Wajumbe zaidi ya 700 wa Mkutano Mkuu wa dharura wa CUF wanakutana mjini Dar es Salaam leo kumchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Ibrahim Lipumba aliyejiuzulu wadhifa huo mwaka jana.

Profesa Lipumba aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho kikuu cha upinzani kuanzia  1995 hadi mwaka, aliachia ngazi kwa kile alichodai kupinga uamuzi wa  viongozi wa vyama vinavyounda Ukawa kumpokea 

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.