Akutwa na kichwa cha binadamu uvunguni

Muktasari:

Tukio hilo limetokea wilayani Chato ambapo Polisi wanachunguza

Chato. Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linawashikilia watu wawili akiwamo mwenye umri wa miaka 65 kwa tuhuma za kukutwa na kichwa cha binadamu nyumbani kwake.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Daniel Shilla akizungumza mjini hapa leo, alisema waliokamatwa ni mkazi wa kijiji cha Ibondo B na mkazi wa Mwabasabhi wilayani Chato.

Alisema tukio hilo lilitokea Septemba 8,  ambapo watuhumiwa hao walikua wamekificha kichwa hicho uvunguni mwa kitanda nyumbani kwa mmoja wao.