Magufuli aitatua papo kwa hapo kero ya kiwanda cha mvinyo

Muktasari:

Ni wakati akisikiliza kero za wadau katika mkutano wa TNBC


Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuruhusu chupa za mvinyo zilizozuiliwa bandarini kwa  sintofahamu ya masuala ya kodi

Akizungumza leo Jumatatu Machi 19, Rais Magufuli ameitaka TRA kumpa mmiliki wa kiwanda cha mvinyo cha Dodoma chupa zake kwa kodi ya bei iliyoinunulia.

“Haya TRA mpeni chupa zake za mvinyo kwa kutoza kodi ile anayodai amenunulia chupa hizo,” ameagiza.

Akiwasilisha kero hiyo, mwakilishi wa kiwanda hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Minde, amesema chupa zake zimekwama bandarini kwa sababu anadaiwa kodi kubwa kuliko uhalisia wa aliyonunulia bidhaa hiyo.

 

Amesema ingawa amewaonyesha risiti lakini wamekataa kumpa mzigo huo, kwa sababu kodi anayodaiwa ni kubwa.