Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mvua yasababisha JPM achelewe kuzindua kiwanda -VIDEO

Muktasari:

Uzinduzi wa kiwanda hicho ulipangwa kufanyika saa nne asubuhi, lakini mvua iliyonyesha kwa zaidi ya saa moja imechelewesha uzinduzi huo


Morogoro. Mvua kubwa iliyonyesha kwa saa moja imefanya shughuli ya uzinduzi wa kiwanda cha sigara cha Philip Moris zichelewe kuanza, huku wananchi mkoani Morogoro wakikubali kulowa kwa ajili ya kumsubiri Rais John Magufuli kufika kiwandani hapo.

Wananchi na viongozi waliohudhuria katika uzinduzi huo walianza kuwasili katika viwanja hivyo leo Alhamisi Machi 15,2018 kuanzia saa 2 asubuhi.

Pamoja na kunyesha mvua kubwa hali ya ulinzi umeimarishwa katika viwanja hivyo na baada ya kukatika, shughuli hizo za uzinduzi ziliendelea kama zilivyopangwa.