Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Diamond awakimbiza Burna Boy, Davido

Muktasari:

  • Mafanikio hayo yanapelekea Diamond kuwaburuza wasanii mbalimbali wenye ngozi nyeusi wa Afrika akiwemo Burna Boy, Davido na Wizkid. 

Nyota wa muziki wa Bongo Fleva Diamondplatnumz amekuwa msanii wa kwanza Afrika mwenye ngozi nyeusi kufikisha wafuasi milioni 8.66 kapitia mtandao wa YouTube.

Mafanikio hayo yanapelekea Diamond kuwaburuza wasanii mbalimbali wenye ngozi nyeusi wa Afrika akiwemo Burna Boy, Davido na Wizkid. 

Msanii anayefuata baada ya Diamond kuwa na wafuasi wengi ni Burna Boy akiwa na 4.65 milioni, akifuatia Davido 3.88 milioni, Wizkid 2.99 milioni na Asake akiwa na wafuasi 1.09 milioni.
 
Aidha katika orodha iliyotolewa na tovuti ya ‘Pan African’ imeonesha kuwa mwanamuziki Diamond ni msanii wa tano kuwa na wafuasi wengi kwa Afrika nzima. Huku namba moja ikishikwa na Muigizaji na mwanamuziki wa Misri Mohamed Ramadan mwenye asili ya Kiarabu ambaye anaupiga mwingi kwenye nyimbo za Kiarabu akiwa na wafuasi 15.4 milioni.