Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

500 kushiriki Kongamano kujadili uchumi jumuishi kuelekea Dira Maendeleo ya Taifa 2050

Mwenyekiti  wa Kongamano  la Mgoda na Kigoda  cha Mwalimu  J.K Nyerere  cha Uprofesa  kutoka Taaluma  ya Umajumui wa Afrika Prof,  Alexander Makulilo (katikati) akizungumza  na waandishi  wa habari kuhusiana  na kongamano  la kujadili  Dira ya Maendeleo  ya Taifa 2050. Picha na Hawa Mathias

Muktasari:

  • Kongamano hilo limeandaliwa  na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana  na Kituo cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi (PPP Centre),litakalo fanyika  kesho Septemba  18, mwaka huu katika Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Mbeya. 

Mbeya. Wadau wa sekta  binafsi, Asasi za kiraia wananchi na viongozi  wa Serikali  wakiwepo wakuu wa mikoa na Wilaya  kushiriki  kongamano  la kujadili  mwenendo  wa kiuchumi wa Tanzania  kuelekea  Dira ya  Maendeleo ya Taifa 2050.

Hatua  ni  kutekeleza  maagizo sita   yaliyo tolewa na  Rais Samia Samia Suluhu Hassan   Julai 17,  mwaka huu wakati akizindua  Dira ya Maendeleo  ya Taifa 2050 jijini Dodoma. 

Kongamano  hilo limeandaliwa  na  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana  na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi  (PPP Centre),litakalo  fanyika katika Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Mbeya.

 Hayo yamesemwa na Mwenyekiti  wa Kongamano  na Mgoda wa Kigoda cha Uprofesa wa  Mwalimu J.K  Nyerere kutoka Taaluma za Umajumui wa Afrika (Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam) Profesa Alexander  Makulilo,  leo Jumatano  Septemba  17,2025. 

Makulilo amesema lengo la kuandaa  kongamano  hilo ni kuwakutanisha wadau  wa sekta mbalimbali zikiwepo  binafsi, asasi zisizo za kiserikali ,vyuo vikuu , washirika wa maendeleo na wananchi lengo  likiwa ni kujadili  kwa kina juu ya fursa za mwenendo  wa kiuchumi nchini  Tanzania  kuelekea Dira 2050.

Amesema awali,  Rais Samia Suluhu  Hassan baada ya kuzindua  Dira hiyo alitoa maelekezo sita  kutaka wananchi,watendaji  na wadau wapatiwe elimu ili kuwezesha kushiriki kikamilifu katika kuchangia .

"Miongoni mwa maagizo  ushirikishwaji  kwenye  utekeleza wa mpango kwa  kuweka mikakati ya Mawasiliano  ya elimu kwa umma na uhamasishaji kuhusu dira ili watendaji  na wananchi waelewe nafasi. na mchango wao,"amesema .

Kuhusu  kuanza utekelezaji  wake.

Makililo amesema Dira  hiyo itaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha Julai  Mosi 2026 huku mpango  wa maandalizi  ya bajeti utaanza mwishoni mwa mwaka 2025 ili wananchi , watendaji na wadau waweze kushiriki  katika utekelezaji  wake  kupitia bajeti mpya ili waweze kutoa mapendekezo.

" Tanzania itakuwa na mpango wa maendeleo wa Taifa kwa miaka mitano  kuanzia 2025/26 mpaka 2029/30 ambao utajengwa kwa kuzingatia hali halisi ya utekelezaji wake,"amesema.

Profesa  ,Makulilo  amesema kuwa  katika kongamano hilo miongoni mwa mada zitakazo jadiliwa ni pamoja na madhumuni ya dira ya 2050 na misingi ya uchumi jumuishi kuelekea mpango  huo na kuangazia mafanikio ya  utekelezaji wa maendeleo  ya Taifa kwa miaka mitano ambayo inaishia 2020/21mpaka 2025/2026.

Nyingine ni nafasi ubia katika uchumi kama msingi wa maendeleo jumuishi na endelevu  nchini Tanzania  huku wachokoza mada wakiwa ni Katibu Mtendaji  wa Tume ya Mipango ,Dk Fredy Msemwa na  Mkurugenzi  mtendaji  wa Kituo  cha Ubia cha Sekta  Binafsi na Umma,David Kafulila.

Wengine ni Mbunge wa Afrika Mashariki,  Gradness Salema ,Mtendaji  Mkuu,Jumuiya ya Wafanyabiashara kundi la  wanawake,  Dk Mwajuma Hamza ,sambamba na Prof,  Humphrey Moshi kutoka Chuo Kikuu cha Dar  Es Salaam.


Kwa upande wake Mratibu  wa Miradi  ya Ubia kutoka  Mamlaka za Serikali  za Mitaa Tanzania  Bara,Msoloni Dakawa amesema wanatarajia ushiriki  wa wakuu wa mikoa wa Mbeya  na Songwe  sambamba  na  Wakuu wa  Wilaya  10.

Wengine  ni wakurugenzi  12 kutoka halmashauri kutoka Mbeya na Songwe ,lakini wapo Makatibu  Tawala wa viwanda uchumi na uzalishaji,Kamishna  msaidizi wa ardhi,wakuu wa idara ya maendeleo  ya jamii,wakuu wa idara 228 .

"Pia, itahususisha  wanasiasa na wazee wa mila (machifu) ,viongozi wa dini ,vijana na wananchi wa kawaida lengo  ni kutekeleza  maagizo  ya Rais Samia Suluhu  Hassan kufikia makundi yote katika kuchangia  Dira ya Maendeleo ya Uchimi wa Taifa ifikapo 2050, "amesema.

Kauli za wadau.

Mkazi wa Jijini hapa na kijana Mhitimu wa elimu ya juu ,Alex Mturo amesema ujio wa kongamano  hilo lije na suruhisho  la changamoto  ya fursa za changamoto  ya kiuchumi,ajira kwa vijana ifikapo 2050,"amesema. 

Mwisho.