Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Adhana yamsimamisha Kenyatta kusoma hotuba Dodoma

New Content Item (1)
Adhana yamsimamisha Kenyatta kusoma hotuba

Muktasari:

  • Rais wa Kenya,  Uhuru Kenyatta amesimamisha hotuba yake kwa zaidi ya dakika moja kupisha wito wa swala (adhana) ya adhuhuri wakati akitoa salamu za pole kwa Watanzania katika shughuli ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Dodoma. Rais wa Kenya,  Uhuru Kenyatta amesimamisha hotuba yake kwa zaidi ya dakika moja kupisha wito wa swala (adhana) ya adhuhuri wakati akitoa salamu za pole kwa Watanzania katika shughuli ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Wakati akianza kutoa salamu zake katika uwanja wa Uhuru jijini Dodoma adhana ilisikika kutoka katika msikiti uliopo karibu na uwanja huo na kumfanya kiongozi huyo kusitisha kwa muda kutoa hotuba yake na adhana ilipomalizika aliendelea na maelfu ya watu waliopo uwanjani hapo walimpigia makofi.

Katika hotuba yake Kenyatta amemwomba Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuendeleza falsafa ya Hapa Kazi Tu aliyoiacha Magufuli kwa kuwa inawafanya Watanzania kuwa na moyo wa ushujaa na kusonga mbele.

Amemtaka Rais Samia kujipa moyo wa ushujaa bila kuteteleka na kuwa Kenya itakuwa pamoja naye wakati wote.

"Katika maandiko ya Biblia Mungu alimwambia Joshua kuwa ‘uwe hodari na moyo wa ushujaa na usiogope kokote uendako Mungu yu pamoja nawe’," amesema Uhuru.

#LIVE: Kuagwa hayati John Magufuli Kitaifa Dodoma

Amesema enzi za uhai wa Magufuli walizungumza kuhusu maendeleo  na usalama wa nchi hizo mbili.

Rais Kenyatta amezungumzia maamuzi aliyokuwa akiyafanya Magufuli kuhusu miradi mikubwa aliyoifanya nchini mwake badala ya kutegemea watu wa nje.