Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

BOT yapokea noti zinazodaiwa ‘chuma ulete’

Muktasari:

  • Benki Kuu Kanda ya Kusini imesema kuwa imekuwa ikipokea pesa zilizochakaa kwa ajili ya kuzibadilisha zikiwemo noti zilizokatwa katika pembe nne ambazo huhusishwa na imani za kitamaduni yaani ‘chuma ulete’.

Lindi. Meneja Huduma za Kibenki wa Benki Kuu Kanda ya Kusini, Melchiades Rutayebesibwa amesema fedha zilizochakaa zimekuwa zikirudishwa ili kubadilishwa ambapo zipo zilimwagikiwa rangi, zilizoandikwa na zingine huja zikiwa zimekatwa katika pembe nne.

Akizungumza katika mahojiano maalumu yaliyotokana na maswali aliyoyauliza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini alipotembelea katika banda la maonyesho ya Nanenane katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi. Alihoji kwanini baadhi ya benki za biashara zinatoa fedha zilizochakaa kwa wananchi.

Amesema kuwa katika mapokezi ya fedha chafu huwa wanapokea zilizomwagikiwa na rangi, zilizochorwa au kukatwa kwenye pembe nne za noti kwa imani za kitamaduni (chuma uletee) na zingine huunganishwa kwa gundi.

"Kuna wakati zinakuja fedha kubadilishwa zingine zinakuwa zimemwagikiwa rangi, zingine zimechorwa au kukatwa kwenye kingo nne za noti zake kwa imani za kitamaduni (chuma uletee)," amesema Rutayebesibwa.

“Unajua moja ya sera ya Benki Kuu ni kuhakikisha wakati wote uwepo wa fedha safi katika mzunguko wa fedha hapa nchini na ikumbukwe Benki Kuu kupitia Sheria ya Fedha ya Mwaka 2006 inawajibu wa kutengeneza pesa za Kitanzania,” amesema Rutayebesibwa.

“Tunazisambaza fedha za Kitanzania hapa nchini kupitia mabenki ya biashara kwa kuondoa fedha zote kwenye mzunguko hapa nchini hasa zilizochakaa ama zilizoharibika au aina yoyote ya uharibufu,” amesema Rutayebesibwa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amehoji kwanini BoT wanaruhusu fedha chafu zilizochakaa kutolewa ndani ya benki za biashara," amesema.


“Kuna wakati unachukua fedha katika benki za huko vijijini mpaka unajiuliza hii pesa imetoka benki kweli zipo baadhi ya benki unakuta wanapesa safi mpaka unapenda ukatoe mara kwa kwa mara huko,” amesema Sagini.

“Lakini kuna vibenki huko sijui wakileta mnawapiga faini nahisi ndiyo maana wanaogopa kuleta. Unakuta benki ipo kijijini ukitoa fedha unachanganyikiwa ilivyochafu, wakati sisi tunaamini kuwa fedha ukitoa benki lazima iwe safi,” amesema Sagini. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania Tawi la Mtwara, Nassor Omari amesema kuwa huwa wanaweka muda maalumu ambao benki za kibiashara hukusanya na kichambua fedha zilizochakaa na kuzirudisha ambapo hupewa mpya.

“Kabla hawajaleta kwetu wanakaa na kuzichambua ili zilizosafi zinabaki na zilizochakaa zinarejeshwa Benki Kuu ili kupata mpya kama zipo zilizochakaa na wanazitoa kwa wananchi hilo ni tatizo  la benki za kibiashara,” amesema Omary.