Maisha ya Malkia Elizabeth II
Muktasari:
- Kumbukumbu za Uingereza zinamtaja Malkia Elizabeth wa pili kama mtawala aliyeongoza Taifa lililounganisha visiwa mbalimbali kwa muda mrefu zaidi ikilinganishwa na watangulizi wake wa awali.
Dar es salaam. Kumbukumbu za Uingereza zinamtaja Malkia Elizabeth wa pili kama mtawala aliyeongoza Taifa lililounganisha visiwa mbalimbali kwa muda mrefu zaidi ikilinganishwa na watangulizi wake wa awali.
Kiongozi huyo wa kimila amefariki jana Alhamisi, Septemba 8, 2022 akiwa na miaka 96 huku akishikilia rekodi ya kuliongoza Taifa hilo kwa muda wa miongo saba.
Elizabeth alianza kuliongoza taifa hilo akiwa na miaka 25 tu mwaka 1952.
Utawala wake wa muda mrefu ulipitia changamoto mbalimbali ambazo mara kadhaa zilisababishwa na mabadiliko ya dunia ambayo iliilazimu Uingereza kutoka kwenye utawala wa kifalme uliojikita haswa kwenye masuala ya kivita hadi kuwa Taifa la kisasa la kitamaduni ambalo liliheshimu uongozi wa kimila lakini maamuzi mengi yakikabidhiwa mikononi mwa waziri mkuu ambaye alitokana na vyama vya siasa.
Mwananchi imekuandalia kumbukumbu za picha za nyakati tofauti ambazo malkia Elizabeth alizipitia kabla na baada ya kupata wadhifa huo mkubwa wa kiuongozi nchini humo.