Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mfanyabiashara akutwa amejinyonga Arusha

Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha, Jonathan Shana 

Muktasari:

  • Mfanyabiashara wa mitumba katika soko la Chini ya mti jijini Arusha, Kelvin Didas (26) amekutwa amekufa kwa kujinyonga leo asubuhi jirani na nyumbani kwake.

Arusha. Mfanyabiashara wa Mitumba na Mkazi wa Sanawari Mtaa wa Texas jijini hapa, Kelvin Didas (26) anadaiwa kujinyonga hadi kufa eneo la jirani na nyumbani kwake.

Mke wa mfanyabiashara huyo, Jack Denis amesema mumewe hakurudi nyumbani usiku wa kuamkia  leo  Jumapili Februari 2, 2020 kutokea kazini na yeye hakushtuka maana huwa ni kawaida yake  siku zingine kutorudi   nyumbani akijua wamefuata mzigo mkoani Tanga.

Akizungumza na Mwananchi, amesema mapema leo asubuhi alipata taarifa kutoka kwa jirani yake aliyefika nyumbani kwake na kumuulizia alipo mumewe naye alimjibu hajarudi tokea jana.

“Nikaambiwa nitoke nje nielekee eneo alipo, nikamkuta tayari amekufa akiwa amenyongwa na nguo zake,” amesema.

Marehemu ameacha mtoto mmoja anayejulikana kwa jina la amani Kelvin (2) .

Akizungumzia tukio hilo, Balozi wa mtaa huo, Elizabeth Thimos amesema leo asubuhi Saa 2 kasoro robo alifuatwa na mama anayejulikana kwa jina la mama Winner  na kumueleza kuwa kuna mtu amekufa, akachukua hatua ya kumtafuta mwenyekiti wa kitongoji hicho lakini hakupatikana  .

Balozi aliendelea kusema baada kutompata kiongozi mwenzake ndipo alipochukua hatua ya kutoa taarifa kituo cha Polisi cha Mjini kati ambao walifika na kuuchukua  mwili kwa ajili ya uchunguzi zaidi pamoja na kuuhifadhi.

Hata hivyo, haijulikani kama marehemu alijinyonga mwenyewe ama amenyongwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha, Jonathan Shana amethibitisha kupata taarifa za tukio hilo na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.