Mke wa Sabaya amaliza kutoa ushahidi kesi ikiahirishwa kwa muda

Watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi akiwemo aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya na wenzake sita wakizungumza na Mawakili wanaowatetea katika kesi hiyo (Picha na Janeth Mushi).

Muktasari:

Mke wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, Jesca Thomas amemaliza kutoa ushahidi leo Januari 18, 2022 baada ya kumaliza kuulizwa maswali ya dodoso na jopo la Mawakili watano wa Jamhuri.

Arusha. Mke wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, Jesca Thomas amemaliza kutoa ushahidi leo Januari 18, 2022 baada ya kumaliza kuulizwa maswali ya dodoso na jopo la Mawakili watano wa Jamhuri.

Jesca ambaye ni shahidi wa pili wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi namba 27/2021 inayomkabili Sabaya na wenzake sita alianza kutoa ushahidi jana katika kesi ambayo inaendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa upande wa washitakiwa kujitetea.

Baada ya shahidi kumaliza ushahidi wake Wakili wa utetezi Mosses Mahuna aliielza mahakama kuwa shahidi anayefuata ni mtuhimiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Sabaya ambaye anaanza kujitetea.

Hakimu Patricia Kisinda anasema anaahirisha kesi kwa dakika tano kisha mahakama kurejea.

Jana Jumatatu akiongozwa na Wakili Mosses Mahuna anayemtetea Sabaya, Jesca alijitambulisha mahakamani hapo kuwa ni mke wa mshitakiwa huyo na walifunga ndoa mwaka 2018.

Hata hivyo jana Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ofmed Mtenga hakumaliza kumhoji shahidi ambapo kesi iliahirishwa mpaka leo ambapo mahojiano yaliendelea.


Hapa ni sehemu ya muendelezo wa maswali ya dodosoa ya Wakili Ofmed Mtenga na shahidi;


Wakili: Unaelewa maana ya kuapa mhkmn kabla ya kutoa ushahidi


Shahidi: Naelewa

Wakili: Unaelewa ukisema uongo mahakamani unaweza ukafunguliwa kesi ukafungwa miaka 5

Shahidi: Naelewa

Wakili: Hebu tutajie ile namba ambayo ulisema ulikuwa unatumia 22.1.2021

Shahidi: 0758 707171

Wakili: Wewe hujawahi kuisajili hii namba

Shahidi: Ndio

Wakili: Lengai Ole Sabaya ndiye aliyesajili


Shahidi: Ndio


Wakili: Na pia tutajie namba ya gari ile ambayo ulisema unaendaha ile VX masai

Shahidi: T 341 ANT


Wakili: Na ulisema hii gari ulinunua baada ya kuanza kuiahi na Sabaya

Shahidi: Ndio


Wakili: Mlinunua Sh ngapi?


Shahidi: Ilinunuliwa zaidi ya mil 15 lakini haikufika Milioni 20


Wakili: Hukumbuki kwa sababu hukununua wewe si ndio?


Shahidi: Tumenunua kwa pamoja


Wakili: Inakuwaje unasahau bei uliyonunua?


Shahidi: Umepita muda mrefu ndo maana

Wakili: Ulinunua kwa nani ile gari?


Shahidi:Ilikuwa kampuni ya ujenzi



Wakili:Inaitwaje


Shahidi:Sikumbuki lakini ilikuwa kampuni ya ujenzi



 Wakili:Mliuziana sehemu gani?


Shahidi:Arusha



Wakili:Arusha sehemu gani Arusha ni kubwa?


Shahidi:Tulikutana kwa Wakili



Wakili:Wakilk gani?


Shahidi:Panaitwa Haraka Law



Wakili:Mwanasheria aliyesaini kwenye hiyo Haraka law alikuwa nani?


Shahidi:Simkumbuki jina



Wakili:Wewe simu unayotumia ni namba ngapi ua kwako nyingine zaidi ya ile nyingine


Shahidi:0754 552520



Wakili:Hii namba uliyotaja ilisajiliwa kwa jina lako wewe?


Shahidi:Mwanzoni ilikuwa imesajiliwa kwa jina langu ila ilipokuja sheria ya kusajili kwa namba ya Nida alinisajilia Lengai  kwani sikuwa na namba ya Nida



Wakili:Kwa hiyo kule anasomeka nani?


Shahidi:Itasomeka Lengai



 Wakili:Wewe hauna mkopo wowote benki


Shahidi:Ndiyo



Wakili:Sabaya pia hana mkopo


Shahidi:Sifahamu hilo



Wakili:Hufahamu mambo ya mume wako?


Shahidi:Huwezi ukayajua yote



Wakili:Katika kipindi mmeishi umewahi kuona amekopa?


Shahidi:sijui na kusikia sijawahi



Wakili:Unaijua namba ya gari ya serikali aliyokuwa anatumia?


Shahidi:Mi najua ni STK sijawahi ku focus kujua namba

Wakili:Unakubaliana na mimi Sabaya ni mtu maarufu sana


Shahidi:Ndiyo


Wakili:Ni kweli kwamba 22.1.2021 mume wako alivyoondoka asubuhi haujui ni kitu gani alichokifanya huko alipokuwa


Shahidi:Mi najua alienda ofisini


Wakili:Ulikuwa naye ofisini


Shahidi:Sikuwa naye



Akihojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tarsila Gervas sehemu ya mahojiano ilikuwa kama ifuatavyo:


Wakili: Jesca kama binti unajua haki zako ni zipi kama mwanamke,mke unazifahamu?


Shahidi:Ndiyo


Wakili:Ni kweli wewe kama mtoto wa kike unayo haki ya kumiliki mali?


Shahidi:Ndiyo



Wakili:Ni ukweli kwamba haki hiyo ni pamoja na mali hizo kuwa kwenye jina lako?


Shahidi:Ndiyo


Wakili:Na ni ukwlei kwamba kati ya mali zote mnamiliki na Sabaya hakuna uliyosema mnamiliki pamoja?


Shahidi:Siyo zote.VX  Masai namba T 341 ANT ina jina langu


Wakili:Na Jesca turudi kwEneye hii gari,hii kampuni ya ujenzi iko wapi?


Shahidi:Iko Arusha



Wakili: Na jina la Jesca kwenye hii gari bila shaka TRA ndivyo lilivyo


Shahidi:Ndiyo


Wakili:TRA linasomeka kama nani?


Shahidi: Jesca Thomas



Wakili:Wewe ni wa wapi


Shahidi:Adress yangu ni 61 Usariver



Wakili:Na huu umiliki ulibadilisha lini toka kampuni hii ya ujenzi kuja kwako


Shahidi:Nilibadilisha tu baada ya kununua,2019 mwanzoni



Wakili:Hii 2019 ulikuwa ukiishi wapi?


Shahidi:Bomang'ombe



Wakili:Jana ulisema hufahamu kuhusu minara ya simu?


Shahidi:Ndiyo sifahamu



Wakili:Na bila shaka wakati unaongea na ile namba 0758 707171 ulikuwa unaendesha gari si ndiyo?


Shahidi:Ndiyo



Wakili:Na bila shaka ile siku kulingana na ushahidi wako wa jana uliongea na watu wawili au watatu?


Shahidi:Niliongea na watu wengi



Wakili:Na uliandika meseji ngapi kutumia ile simu?


Shahidi:Sikumbuki ni ngapi



Wakili:Na hii simu uliita ya biashara imesajiliwa kama ya biashara na siyo mtu binafsi


Shahidi:Tulisajili kama mtu binafsi



Wakili: Hii simu ilisajiliwa lini?


Shahidi: 2018 mwishoni



Wakili:Na ni vitu gani vilitumika kusajili


Shahidi:Aliyesajili ni Lengai 



Wakili:Hukujua ametumia nini kusajili si ndiyo?


Shahidi:Eeeh



Wakili:Na ni ukweli appartment mliyokamatwa ina stairs kwa juu?


Shahidi:Ilikuwa hotelini ghorofa ila siyo apartment



Wakili:Na ilikuwa Mbezi si ndiyo?


Shahidi:Ndiyo



 Wakili:Unafahamu watu wangapi wanaofanya kazi na mume wako


Shahidi: Namfahamu aliyekuwa DAS wake na Mkurugenzi,dereva na mdada alikuwa DMO ndiyo watu walikuwa wanakuja nyumbani

Wakili:Ndugu yako anaishi kwa Morombo anaitwa nani?


Shahidi:Morombo sina ndugu



Wakili: Kwa kuwa kwa mila zao huruhusiwi kuingilia masuala hayo ya kuuza mifugo au namna mume wako anapata hela  hela inayokuja hujui imetokana na nini?


Shahidi:Siyo kweli hela inayokuja najua imetokana na kuuza mifugo



Wakili:Akienda kupora


Shahidi:Hajawahi kwenda kupora



Wakili:Turudi kweye mifugo na hujihusishi kwenye mifugo akikuaga anaenda kuuza mifugo na hajauza si kweli huwezi kujua?


Shahidi:Mara nyingi tunafatana



Wakili:Ushuru wa mifugo ile mliyouza Milioni 20,mlilipa kiasi gani?


Shahidi:Inategemea na idadi na bei za ushuru ni kuanzia 1000 hadi 5000 inategemea na mnada ni upi ila sijui kwa sababu mimi sikwenda mnadani



Wakili:Fomu ya maadil ya mume wako ulikaa nayo muda gani kabla ya kupeleka Takukuru kama ulivyosema jana?


Shahidi:Ilijazwa 12/2020.Alikuja nayo ilikuwa ndani


Wakili:Inafananaje hiyo fomu


Shahidi:Ni fomu tu



Wakili:Wewe ulifahamuje ni fomu ya maadili?


Shahidi:Niliambiwa tafuta documebt zote leta ya fomu ya maadili



Wakili:Sasa baada ya kuitafuta umeipata katika kuiangalia inafananaje?


Shahidi:Mimi sikuikagua.Niliambiwa kuna kopi imeandikwa fomu ya maadili




Wakili: Uliyotoa PCCB ni kopi ama origional


Shahidi:Mimi sijui kopi wala origional


Wakili:Labda utukumbushe uliwapa PCCB vitu gani vingine?


Shahidi:Gari VX T 341 ANT,file ya gari namba T 222 BDY ilikuwa na jina la Lengai ndani kulikuwa na mkataba wa mauziano na kadi


Wakili:Hiyo kadi mlipata lini toka TRA?


Shahidi:Sikumbuki


Wakili:Mlinunua lini hilo gari?

Shahidi:Ilikuwa 2020


Wakili:Kingine mlichotoa


Shahidi:Fedha


Wakili:Kiasi gani


Shahidi:Ilikuwa siyo chini ya Milioni 10


Wakili:Mlitoa wapi hizo fedha?

Shahidi: Zilitolewa kwenye akaunti ya biashara 


Wakili:Iko benki gani?

Shahidi: CRDB


Wakili:Mlizitoa lini

Shahidi:Sikumbuki lakini tulizitoa tukiwa Dar


Wakili:Kingine?


Shahidi:Simu


Wakili:Ilikuwa simu gani?

Shahidi:Samsung moja ilikuwa Iphone


Wakili:Laini zilizokuwa kwenye hizo simu tuanze na Samsung?

Shahidi: 0758 707171


Wakili: Iphone?

Shahidi: 0754 552520

Wakili:Hii Iphone yenye namba 0754 552520 na wewe ndiyo unatumia?


Shahidi:Ndiyo


Wakili:Unajua majukumu ya mume wako aliyokuwa akiyafanya ya kazi?


Shahidi: Mi najua ni Mkuu wa Wilaya



Wakili:Alikuwa anatakiwa ahakikishe sheria zinafuatwa na yeye pia asivunje aheria na aliapa kufanya hivyo,


Shahidi: Ndio


Wakili:Upendo Wilfred Mbise ni nani?


Shahidi: Simfahamu



Wakili: Jesca Thomas Nassari ni nani


Shahidi: Mimi



Hakimu umesema nani?


Wakili: Upendo Wilfred Mbise mtoto wa mjomba wako hamfahamu



Wakili: Ni kweli Sylvester hujawahi kumuona katika maisha yako?


Shahidi: Simfahamu


Wakili: Kuna mtu ambaye mlikamatwa naye Dar na mlikuwa chumbani yeye alikuw sebuleni humfahamu?

Shahidi: Hapana


Wakili: Unampenda sana mume wako si ndiyo?


Shahidi: Ndiyo


Wakili: Kwanini uliwaambia Takukuru Arusha 4/6/2021 Sabaya ni mchumba wako siyo mume wako?


Shahidi: Niliwahi kuhojiwa mara moja kuhusu Sabaya na ni Dar na nilisema ni mume wangu




Wakili: Hata ulivyokabidhi ulikabidhi kama mchumba na siyo mke na ulikabidhi sakina si ndiyo


Shahidi: Hapana


Wakili: Ninkweli Dar mlikabidhi simu na fedha mbali na gari?


Shahidi: Kila mtu alikuwa anakabidhi za kwake


Wakili: Ulikabidhi simu gani Dar Es Salaam?


Shahidi: Samsung na Iphone


Wakili: Ni kweli kwamba utafanya chochote ili mume wako awe huru


Shahidi: Ambacho hakivunji sheria


Wakili:Wakati mwenzangua nauliza ulisema unaelwqa maana ya kusema uongo mahakamani si ndiyo


Shahidi: Ndio


Wakili: Kuan mchunganmji ulimtaja alifunga ndia yenu ni nani?


Shahidi: Anaitwa Dk Lekundayo


Wakili: Ni wa wapi?


Shahidi: Ni mchungaji na Askofu Arusha Central Churu


Wakili: Tangazo la kwanza la ndoa yenu lilikuwa tarehe ngapi?

Shahidi: Sikumbuki


Wakili: lilitangaza mara ngapi?

Shahidi: Mara tatu

Wakili:Kati yako na mume wako nani muumini wa hilo kanisa?


Shahidi: Yeye na mimi baada ya kufunga ndoa


Wakili: Kabla ya hapo ulikuwa muumini wa kanisa gani?


Shahidi: Lutheran huko Meru



Wakili: Yale maghala yako yako wapi?


Shahidi: Kisongo, Morombo na Tengeru


Wakili: Unanunua wapi hayo mazao?


Shahidi: Nanunua mashambani Loksale, nalima na nanunua Loksale


Wakili: Lengai mara ya kwanza umemuona wapi?


Shahidi: Arusha


Wakili: Mwaka gani?


Shahidi: 2016


Wakili: Udom ulimaliza mwaka gani?


Shahidi: 2016


Wakili wa Serikali Neema Mbwana naye anaanza kumhoji shahidi


Wakili: Shahidi umesema unaishi wapi?

Shahidi: Kwa sasa naishi Sakina

Wakili: Unaishi na nani?

Shahidi: Naishi mwenyewe

Wakili: Huyo mumeo yuko wapi kwa sasa?

Shahidi: Magereza

Wakili: Si mumeo Magereza anafanya nini

Shahidi: Mhehsimiwa nisingependa kujibu hilo swali

Wakili: Nauliza mumeo yuko wapi kwa sasa?

Shahidi: Nikasema magereza

Wakili: Kwanini anaishi Magereza ni mfungwa au mahabusu?

Shahidi: Kama mahabusu kwenye hii kesi

Wakili: Shahidi umesema wewe ni mjasiriamali toka lini?

Shahidi: Toka 2018

Wakili: Imeleta kitu gani umeleta hapa mahakamani kuthibitisha wewe ni mfanyabiasha wa maharage na mahindi?

Shahidi: Sijaleta ikihitajika naleta

Wakili: Shahidi umeshasema uongo mara ngapi hapa mahakamani?


Shahidi: Sijasema uongo

Wakili: Kumbukumbu za biashara yako unaweka wapi?


Shahidi: Inayohitajika nyumbani inakaa nyumbani,inayokaa stoo inakaa stoo

Wakili: Umeleta hapa mahakamani?

Shahidi: Nimesema sijaleta zikihitajika nitaleta


Wakili: Malula unamiliki kiasi gani cha ardhi?

Shahidi: Malula shamba ni kubwa sihawaji kupima


Wakili: Tanga?

Shahidi: eka 11


Wakili: Tanga hizi eka 11 mlinunua kiasi gani?


Shahidi: Na lenyewe nimelikuta


Wakili: Fedha zilizokuwa zinatokana na mauzo ya mifugo zilikuwa zinawekwa wapi?


Shahidi: Nyingine zinawekwa benki CRDB, zingine zinafanyia mambo mengine


Wakili: Hiyo akaunti ni ya biashara au binafsi?

Shahidi:I lifunguliwa kama joint akaunti


 Wakili: Mlifungua tawi gani?


Shahidi: Friends Corner


Sasa Wakili wa Serikali Mwandamizi, Janeth Sekulesehemu ya anamhoji kama shahidi ifuatavyo

Wakili: Umeieleza mahakama kwa nyakati tofauti umekuwa ukiambatana na mume wako akienda kuuza mifugo?

Shahidi: Ndio

Wakili: Kutokana na mila ni sahihi ulikiwa huruhusiwi kujua idadi ya mifugo iliyopo na inayouzwa?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Ni sahihi ukiwa kama mke halali wa Sabaya hukuwahi kujua mume wako ana mkopo kama ulivyoeleza mahakama?

Shahidi: Ndio

Wakili: Na wala hukujua nyaraka alizotumia Sabaya laini zile mbili ulizokuwa ukitumia kwa biashara na binafsi?

Shahidi: Sikujua


Wakili: Hujui idadi ya kifuhi, hujui iwapo ana mkopo au hana nitakuwa sahihi nikisema wewe kama mke hukujua kila kitu anachokifanya mume wako akiwa mbali na wewe au akiwa anafanya shughuli nyingine?


Shahidi: Nilijua alivyonishirikisha


Wakili: Kwa maana hiyo hata 22.1.2021 ambayo ulidai ulikuwa Arusba huwezi kujua kama yeye na genge lake walikuja Arusha


Shahidi: Nilimwacha Boma

Wakili: Ndoa mlifunga lini


Shahidi: 27.5.2018


Wakili: Ulibatizwa lini?


Shahidi: Nilibatizwa kabla ya ndoa


Wakili: Ulibatizwa sehemu gani


Shahidi: Ikizu, Musoma

Wakili: Umedai hapa leo wewe umebatizwa Ikizu Musoma, mara ya kwanza ulivyoulizwa swali na Tarsila ulisema ulianza kuabudu Sabato baada ya kufunga ndoa

Shahidi: Ndio


Wakili: Ni sahihi ulisema kabla ya ndoa ulianza kuabudu Lutheran kule Meru


Shahidi: Ndiyo

Wakili: Umesema ulibatizwa Ikizu huko ulibatizwa kwa imani ipi?

Shahidi: Nilibatizwa kuingia Sabato

Wakili: Kwanini ulichagua kwenda Ikizu wakati ulisema unakaa Meru?


Shahidi: Sikuamua mimi mwenyewe tulijadiliana na ni sehemu Lengai alibatizwa

Wakili: Jesca nitakuwa sahihi nikisema tangu umeoana na Lengai hujawahi kuwa na maamuzi yako peke yako?

Shahidi: Kitu kama kinanihusu mimi ninayo,kama kinahusu familia tunajadiliana

Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema hata wewe kuja kutoa ushahidi hasa kusema Januari 22, 2021 simu ulikuwa nayo wewe ni maelekezo uliyopewa kuja kutoa mbele ya mahakama hii

Shahidi: Ilikuwa maamuzi yangu sijaelekezwa


Baada ya shahidi kumaliza kutoa ushahidi wake Wakili wa utetezi Mosses Mahuna aliielza mahakama kuwa shahidi anayefuata ni mtuhimiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Sabaya ambaye anaanza kujitetea.

Hakimu Patricia Kisinda anasema anaahirisha kesi kwa dakika tano kisha mahakama kurejea, kesi imeahirishwa saa 12:35 mchana.