Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Samia ateua Mwenyekiti Tira

Muktasari:

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Moremi Marwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (Tira).

Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Moremi Marwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus imesema uteuzi huo umeanza Mei 14, 2023.

Marwa ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA) pia aliwahi kuhudumu kwa miaka tisa kama Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Mamlaka ya (Tira) ilianzishwa chini ya Sheria ya Bima Na.10 ya mwaka 2009 yenye jukumu la kuratibu sera na mambo mengine yanayohusu bima katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.