Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

RC Kilimanjaro: Wanaomiliki silaha kinyume cha sheria wazisalimishe

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

  •  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amewataka wananchi wa mkoa huo kusalimisha silaha wanazozimiliki kwa njia haramu katika vituo vya polisi au ofisi za Serikali.



Moshi. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amewataka wananchi wa mkoa huo kusalimisha silaha wanazozimiliki kwa njia haramu katika vituo vya polisi au ofisi za Serikali.

Akizungumza na watendaji, wenyeviti wa vijiji  pamoja na makatibu wa mashina wa CCM kwenye semina ya kuwajengea uwezo na kutambua majukumu yao ya kazi amesema adhabu ya kukutwa na silaha kinyume na sheria ni kifungo zaidi ya miaka 15.

"Kama unamiliki silaha ambayo sio yako tafadhali naomba mkazikabidhi silaha hizo kunako husika kabla sheria haijaanza kuchukua mkondo wake,"amesema RC Kagaigai

Naye kamanda wa polisi mkoani humo, Simoni Maigwa ametaka wananchi kutumia muda uliowekwa na Serikali katika kusalimisha silaha hizo kabla ya msako kufanyika.

Amesema Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, George Simbachawene ametoa muda wa mwenzi mmoja kuanzia Novemba mosi hadi 30 mwaka huu wananchi kusalimisha silaha kwa hiari na kwamba baadaye polisi itaendesha msako maalum na hatua za kisheria zitachukuliwa.