Rugemalira atoa sadaka ya shukrani kanisani

Rugemalira atoa sadaka ya shukrani kanisani

Muktasari:

  • Siku tatu baada ya kuachiwa huru mfanyabiashara James Rugemalira, leo Septemba 19 ameungana na waumini wenzake wa parokia ya Makongo Juu kushiriki misa takatifu ya jumapili.

Dar es Salaam. Siku tatu baada ya kuachiwa huru mfanyabiashara James Rugemalira, leo Septemba 19 ameungana na waumini wenzake wa parokia ya Makongo Juu kushiriki misa takatifu ya jumapili.

Mfanyabiashara huyo aliachiwa huru Alhamisi Septemba 16 wiki iliyopita baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka minne.

Katika ibada hiyo Rugemalira akiwa ameambatana na mkewe wametoa sadaka ya shukrani na kumshukuru Mungu kwa kumuwezesha kutoka gerezani.

Akizungumza baada ya kutoa sadaka hiyo, Rugemalira aliwapongeza waumini wenzake kwa kufanikisha ujenzi wa kanisa hilo, kazi iliyofanyika wakati yeye akiwa gerezani.

Kupata habari hii kwa undani soma gazeti la Mwananchi