Sh166 bilioni zatumika elimu bure

Sh166 bilioni zatumika elimu bure

Muktasari:

  • Serikali ya Tanzania imesema hadi kufikia Februari 2021  imetumia Sh166.17 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa elimu msingi bila ada pamoja na kujenga na kukarabati   miundombinu ya elimu nchini.

Dodoma. Serikali ya Tanzania imesema hadi kufikia Februari 2021  imetumia Sh166.17 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa elimu msingi bila ada pamoja na kujenga na kukarabati   miundombinu ya elimu nchini.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Aprili 13, 2021 na Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa wakati akiwasilisha bungeni mwelekeo wa kazi za Serikali na makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2021/22.

Amesema Serikali   imeboresha   miundombinu   ya   shule za msingi   1,372   na   sekondari   554   kwa   lengo   la kuimarisha    ufundishaji na ujifunzaji.

Majaliwa amesema pia Serikali imekarabati  shule  18  za wanafunzi  wenye  mahitaji maalumu na   imeongeza fursa  za  upatikanaji  wa elimu  ya  juu kwa  kutoa mikopo kwa wanafunzi 142,179.

Majaliwa amesema Sh464 bilioni zitatumika kwa mwaka   wa masomo 2020/2021 ikilinganisha  na Sh450 bilioni zilizotumika kwa wanafunzi 130,883 mwaka 2019/2020.