Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Spika Ndugai amuonya Nape kuhusu wabunge 19 Chadema

Ndugai amemuonya Nape kuhusu michango yake bungeni

Muktasari:

  • Spika wa Bunge,  Job Ndugai amemuonya mbunge wa Mtama (CCM),  Nape Nnauye kuchunga kauli zake anapochangia bingeni kuhusu wanawake.

Dodoma. Spika wa Bunge,  Job Ndugai amemuonya mbunge wa Mtama (CCM),  Nape Nnauye kuchunga kauli zake anapochangia kuhusu masuala ya wanawake.

Ametoa onyo hilo leo Jumatatu Mei 3,  2021 alipozungumzia  mchango wa mbunge huyo kuhusu wabunge 19 ambao Chadema imetangaza kuwafukuza uanachama na ambao bado wameendelea kuwa wawakilishi wa chama hicho bungeni.

Hivi karibuni Nape akiwa kwenye mjadala nje ya Bunge alikosoa wabunge hao kuendelea kuwepo bungeni licha ya kufukuzwa Chadema, huku akitaka Katiba ya nchi ifuatwe.

Ndugai amemuonya Nape kuhusu michango yake bungeni

"Hivi karibuni mbunge wa Mtama mdogo wangu Nape Nnauye alitoa mchango wake hapa, Sina haja ya kuzuia uchangiaji wake lakini alikiuka kanuni kwa kuwataja wabunge kwa majina, hapo alikosea sana," amesema Spika Ndugai.