Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tambwe Hiza: Tushindane kwa hoja

Muktasari:

Alisema kukishakua na figisufigisu ndio hapo vurugu zinapoanza kutokea  jambo ambalo chama chao kisingependa yatokee.

Kada wa Chadema, Tambwe Hiza amesema watu wanapaswa kujua uchaguzi sio vita, na kila mmoja anapaswa kushindana kwa haki.

Alisema kukishakua na figisufigisu ndio hapo vurugu zinapoanza kutokea  jambo ambalo chama chao kisingependa yatokee.

Pia Hiza kaonya watu wa Serikali kutowatisha wananchi kwa sababu  wao ndio wamewachagua na kuwaweka madarakani.

Kada huyo amesema  wakati CCM wakisema Salum Mwalimu Mzanzibar mbona hawamsemi Mtulia ambaye ni Mpemba.

"Tunataka wajue hatujaja kushindana hapa kwa makabila  wala udini  bali tumekuja kushindana kwa hoja za chama kipi bora na wanaochagua wanachagua ubora wa mgombea na sio dini wala kabila lake," amesema  Hiza.

"Tunapokuja kwenye kampeni tuangalie mambo ya msingi, na sio ya mtu kusimama na kusema nampenda mtu fulani wakati kuna mamilioni ya wananchi Kinondoni waliokuamini na kuchagua utawaondolea matatizo yanayowakabili," alisema Kada huyo.

Serikali nzima imeshindwa na Bakhresa ambaye anamiliki kiwanda cha unga, meli, sasa kuliko kuichagua CCM si bora kumchagua Bakhresa na kueleza kwamba wasipowachagua Chadema hawawakomoi wanachama wa chama hicho bali wanajioa na wao.