Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tembo yaua watu wawili Tanga

Kamanda wa Polisi mkoani Tanga,  Edward  Bukombe

Muktasari:

  • Ni mwanamke na mwanaume wilayani Korogwe

Korogwe: Watu wawili akiwemo mwanaume mmoja na mwanamke wamekufa baada ya kushambuliwa na Tembo huko katika vijiji viwili tofauti vya Halmashauri ya wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi mkoani Tanga,  Edward  Bukombe alisema  tukio hilo  lilitokea jana  Agusti 19, 2018 saa moja asubuhi  katika kata za Kalalani na Kizara kwenye vijiji  vilivyopo  mpakani  mwa  hifadhi ya mbuga ya Mkomazi.

Kamanda Bukombe  aliwataja  majina  ya watu hao waliokufa kuwa ni Jumaa Kanju (24) mkazi wa Bombo Majimoto, kata ya Kizara  na Habiba  Ramadhani (70) mkazi wa Mtoni Bombo Kalalani. Alisema kuwa watu walishambuliwa  Agosti 19.

 

Alisema kikundi cha Tembo  kiliwashambulia kwa  kuwakanyaga kanyaga  marehemu hao na kusababisha  majeraha sehemu za kichwani, tumboni na miguuni.

 

Aliongeza kusema kuwa miili ya marehemu imezikwa jana baada ya polisi kufika eneo la tukio na kujiridhisha juu ya kile kilichotokea na kutoa ruksa kwa ndugu wa marehemu kufanya maziko.

 

Diwani wa Mashewa, Seif Hillary alisema  tukio kama  hilo  halijawahi kutokea bali tembo hao wanaosadikiwa kutoka hifadhi ya Mkomazi wamekuwa na tabia  kuharibu mazao kwenye mashamba ya wananchi wa vijiji  hivyo.

 

Hillary alisema baada ya tukio hilo waliwataarifu askari wa Tanapa ambao walifika mapema kwenye eneo hilo wakifanya taratibu za kuwarejesha Tembo hao walikotoka.

 

Pamoja na hayo tayari wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari juu ya wanyama hao huku diwani huyo akisema iko haja kwa wanyama hao kuwekewa udhibiti wasiweze kudhuru wananchi.

 

Mkuu  wa  askari  wa  Hifadhi  ya Taifa  Mkomazi, Laurent  Kawau alisema  baada  ya  kupata  taarifa  kutoka  kwa viongozi  wa Kata  ya  Mashewa  waliweza  kutuma  askari  na  magari  katika  eneo  la  tukio

Kawau  alisema  mpaka sasa wamefanikiwa kuwanasaga  Tembo hao kurudi  katika  hifadhi hiyo ya Mkomazi na wengine wameelekea  katika  msitu  wa Mashewa uliopo  mbali  na makazi  ya wanakijiji.

“Tulituma  askari  na magari  kutoka Hifadhi  ya Mkomazi, Tanapa pamoja  na magari matatu  yapo  katika  eneo la tukio “

Alisema  tembo  hawa  kwa  sasa  wanatoka  kutokana  na utulivu  ulipo  (wawindaji  haramu hawapo) hivyo  wanafuata  njia zao  za  zamani  kwani  tembo  hata  kama alipita  miaka  50 iliyopita  lazima  kizazi chake pia kipite  njia  hiyo.

Pia  aliwataka  wananchi  wa maeneo hayo uchukua  tahadhari  kwa  kuacha  kutembea  usiku sana  na asubuhi  pamoja na kuacha kupiga  kelele wawapo barabarani  kwani  tembo  hao  wakisikia kelele  huzifuata sauti  zilipo.