Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Waganga wakuu wapewa maelekezo usimamizi sampuli za vipimo vya VVU

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Jafar Haniu (kushoto) akionyesha ishara ya kupokea mashine ya maabara ya kupimo vya sampuli kutoka kwa  Mkurugenzi Mkazi wa WRAIR, Mark Breda (kulia)kwa ajili ya hosptali za mikoa  ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi. Picha na Hawa Mathias

Muktasari:

  •  Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya, Jafar Haniu amewataka waganga wakuu kusimamia usafirishaji sampuli za maabara na kuimarisha afua za maambukizi ya VVU

Mbeya. Waganga wakuu  wa  hospitali za mikoa  ya Mbeya, Songwe, Katavi na Rukwa  wameagizwa  kusimamia utunzaji na usafirishaji wa sampuli za maabara na  kuimarisha  afua  za  maambukizi  ya VVU katika vituo vya kutolea huduma.

Hatua hiyo iende sambamba na kufanya ziara ya kukagua vituo vya afya zahanati zilizofanyiwa  ukarabati kupitia  ufadhili wa PEPFAR kama zinalingana na thamani ya fedha,  na  kuchukua hatua kwa watakao bainika kufanya ubadhirifu.

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe , Jafar Haniu ametoa maelekezo hayo  leo Alhamisi Juni 6,2024 alipokuwa  akipokea vifaa  vya maabara  vyenye thamani ya zaidi ya Sh132.9 milioni kwa ajili ya Hospitali za Mikoa ya Mbeya, Songwe, Katavi na Rukwa.

Vifaa hivyo vimetolewa  kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani (PEPFAR) kupitia  WRAIR na HJFMRI kwa lengo la kutekeleza afua za mapambano dhidi ya Ukimwi.

"Waganga wakuu kasimamieni hospitali zote  zinazonufaika  kupitia  HJFMRI kwa kutekeleza afua za VVU ikiwamo ajira kwa watumishi wa kada za afya kwa lengo kutekeleza mapambano dhidi ya Ukimwi sambamba na ukaguzi wa vituo  ya afya na zahanati  "amesema Haniu.

Haniu amesema Serikali itaendelea kutekeleza afua za Ukimwi katika kuimarisha huduma za maabara katika hospitali, vituo vya afya na zahanati kwa  kushirikiana na wadau.

Kwa upande wake  Mkurugenzi Mkuu wa HJFMRI Tanzania ,Dk Sally Chalamila amesema lengo la kutoa vifaa na mashine za maabara ni kuwezesha watoa huduma kufanya tafiti za sampuli  na kupata tiba za wagonjwa.

Amesema maabara hizo zitaboresha  upatikanaji wa huduma  katika mikoa hiyo  kwa  lengo ni kufikisha huduma kwa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkazi wa WRAIR   ,Mark Breda amesema wataendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya VVU.


"Vifaa hivyo vina thamani ya Sh132.9 milioni vimetolewa  kwa mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi sambamba na mashine ya uchunguzi saratani ya mlango wa shingo ya  kizazi yenye thamani ya Sh30 milioni,"amesema.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk Jonathan Ludemo amesema  vifaa hivyo vya maabara  vitawezesha tija kwa Watanzania na kupata  huduma stahiki.

"Kwa niaba ya wenzangu mikoa ya nyanda za juu kusini tumeona jinsi gani wadau  wanaboresha upatikanaji wa  huduma za uchunguzi wa sampuli  za magonjwa mbalimbali katika kufikisha huduma kwa jamii, "amesema.