Wahamiaji haramu 47 wafikishwa mahakamani
Muktasari:
- Wahamiaji haramu raia wa Ethiopia 47 wamefikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.
Moshi. Wahamiaji haramu raia wa Ethiopia 47 wamefikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.
Wahamiaji hao walikamatwa usiku wa kuamkia jana wamefikishwa mahakamani hapo leo Ijumaa Agosti 12, 2022.
Raia hao walikamatwa katika operesheni maalumu iliyokuwa ikifanywa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na jeshi la uhamiaji mkoani humo.
Hata hivyo, mara baada ya kukamatwa kwa raia hao ambao walikuwa wakiongozwa na mtanzania mmoja, Mkuu wa Mkoa huo, Nurdin Babu aliviagiza vyombo vya sheria mkoani humo kumshughulikia Mtanzania huyo kwa mujibu wa sheria za nchi.
Endelea kufuatilia mitandao yetu kujua kinachojili mahakamani hapo