Wahamiaji haramu 47 wahukumiwa mwaka mmoja jela
Muktasari:
- Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya Sh500,000 kwa kila mmoja wahamiaji haramu 47 raia wa Ethiopia waliongia nchini kwa njia za panya.
Moshi. Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya Sh500,000 kwa kila mmoja wahamiaji haramu 47 raia wa Ethiopia waliongia nchini kwa njia za panya.
Hukumu hiyo imetolewa leo Ijumaa Agosti 12, 2022 na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Jenifa Edward.
Wahamiaji hao walikamatwa usiku wa Agosti 12, katika eneo la Mgagao Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro wakiwa na Mtanzania mmoja mkazi wa Mbeya.
Hata hivyo baada ya kukamatwa kwa wahamiaji hao haramu Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu alivitaka vyombo vya sheria mkoani humo kuchukua hatua za kisheria ili kuwawajibisha wale wote wanaovunja sheria