Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wasakwa kwa kuiba Sh31. 2 milioni kisha kujeruhi walinzi

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Berthaneema Mlay akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uporaji wa fedha kwenye maduka yanayotoa huduma za kifedha kwenye kata ya Nyawilimwilwa wilayani Geita.

Muktasari:

Jeshi la Polisi mkoani Geita linawasaka watu wasiojulikana waliovamia na kupora maduka yanayotoa huduma za kifedha katika eneo la soko kata ya Nyawilimwilwa wilaya ya Geita kisha kupora Sh31.2 milioni na kujeruhi walinzi saba waliokuwa wakilinda maduka hayo.

Geita. Kundi la watu 10 wanaosadikika kuwa wezi wamevamia na kupora maduka nane ya huduma za kifedha yaliyopo kata ya Nyawilimwilwa Wilaya ya Geita na kuiba Sh 31.2 milioni kisha kuwajeruhi walinzi saba waliokuwa wakilinda maduka hayo.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Berthaneema Mlay amesema tukio hilo limetokea April 23, 2023 Saa 9 alfajiri ambapo kundi hilo linalodaiwa kuwa la vijana lilivamia eneo la soko na kufanya uhalifu huo.

Amesema kabla ya kuvunja maduka hayo ya huduma za fedha waliwashambulia walinzi kwa kutumia silaha za jadi yakiwemo mapanga ambapo mlinzi mmoja alijeruhiwa kichwani na kitu chenye ncha kali.

“Nitoe wito kwa wananchi kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi ili washirikiane na polisi kuimarisha ulinzi lakini wamiliki wa maduka wekeni walinzi wenye viwango kulinda biashara zenu hawa walinzi  kama wangekuwa na silaha wangeweza kuwadhibiti wahalifu hawa”amesema Mlay

Katika tukio jingine watu watano wakazi wa kata ya Kakola wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuchoma nyuma mbili za Juma Masanja wakimtuhumu kuwa ni mwizi sugu.

Kamanda Mlay amedai watu hao wanadaiwa kuchoma nyumba hizo baada ya kugundua mmiliki hayumo ndani na kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini walioiba kwenye maduka ya huduma za kifedha sanjari na kuwakamata waliochoma nyumba ya Musa ili waweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.