Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Watoto 2,300 wamebakwa

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Muktasari:

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi katika kipindi cha Januari hadi Machi mwaka 2016, matukio 1,765 yaliripotiwa katika vituo mbalimbali vya polisi nchini.

Dodoma/Dar.  Matukio ya ubakaji watoto nchini yameongezeka kutoka watoto 422 mwaka 2014, kufikia matukio 2,358 mwaka jana.

 Hayo yalisemwa bungeni na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alipokuwa akizungumzia maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika leo.

 Ummy amesema kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi katika kipindi cha Januari hadi Machi mwaka 2016, matukio 1,765 yaliripotiwa katika vituo mbalimbali vya polisi nchini.