Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Watoto wafariki kwa kuzama bwawani wazazi wakiwa msibani

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi akizungumzia vifo vya watoto hao

Muktasari:

Watoto wawili wa familia moja katika Kitongoji cha Nkongolo Kijiji cha Kabila Kata ya Mondo Wilayani Kishapu, wamefariki dunia baada ya kuzama kwenye bwawa la maji lililopo jirani na makazi yao.

Shinyanga. Watoto wawili wa familia moja katika Kitongoji cha Nkongolo Kijiji cha Kabila Kata ya Mondo Wilayani Kishapu, wamefariki dunia baada ya kuzama kwenye bwawa la maji lililopo jirani na makazi yao.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kishapu ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mondo, William Jijimya amesema watoto hao waliachwa na wazazi wao nyumbani kisha kwenda  msibani  kwenye kijiji cha Kabila.

Amewataja watoto waliofariki ni Meckline Dioniz (6) na Mbalu Dioniz (3) ambapo amesema wazazi wao waliporudi usiku hawakuwakuta nyumbani na kuanza kuwatafuta, ilipofika saa 4 usiku wakaupata mwili wa mtoto mmoja ukielea juu ya maji na baadaye wakaupata mwili wa mtoto mwingine.

Amesema juhudi za kuwatafuta watoto hao zimefanywa na wazazi kwa kushirikiana na wananchi wa kitongoji hicho baada ya kukusanyika usiku huo na kuanza kutafuta kisha kufanikiwa kuwapata wote wawili .

“Tukio hili limetusikitisha limetokea wakati wazazi wakiwa wameenda msibani na baada ya kurudi wamekumbana na mkasa huo wamepoteza watoto wote wawili  hili nifundisho kwetu sisi wazazi watoto hawakuwa na mtu mzima wa kuwasimamia”amesema Jijimya

Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola wamefika eneo la tukio ambapo miili ya watoto hao imefanyiwa uchunguzi na taratibu zingine kuendendelea.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa watoto hao waliachwa nyumbani bila uangalizi na ndipo wakakumbwa na umauti.