‘Valentaini dei’ pisi kali na mwendo wa vibabu

Muktasari:

  • Waya mkali mwanangu unaanzia watu kuisemesha totozi? Nguruwe pita sina mshale ndiyo msemo wetu.Watu tumekata ringi kitaa tunatembea upande upande kama kaa wa Kilwa Kivinje. Trip moja chooni tripu moja jikoni. Enewei.. mambo vipi? Ishu zikoje, mia mia? au hadithi bado haijabadilika?

Wikiendi iliyopita nilikuwa na mshikaji sehemu tunapiga vyombo. Kama kawa stori ni undezi wa mgawo wa umeme na laifu kwa ujumla. Masela huwa hatuna upimbi wa kusema watu kibwege bwege tu. Ikikatiza pisi kali stori zinakatika kama umeme. Tunaitazama, tunaithaminisha kisha tunaendelea na stori zetu za kilofa lofa tu.

Waya mkali mwanangu unaanzia watu kuisemesha totozi? Nguruwe pita sina mshale ndiyo msemo wetu.Watu tumekata ringi kitaa tunatembea upande upande kama kaa wa Kilwa Kivinje. Trip moja chooni tripu moja jikoni. Enewei.. mambo vipi? Ishu zikoje, mia mia? au hadithi bado haijabadilika?

Na msimuliaji ni yuleyule?

Hadithi za huenda kesho mambo yakawa on line! kesho yetu ya kila siku. Kesho ile ile, kesho isiyofika. Kesho yenye ukenge usiyo na faida. Kila kukicha tunaendelea kuilaumu Serikali na viongozi wake na kutaka kila hoja iwe ya pesa.Najua wapo ambao mko pouwa kama mnaishi peponi. Sisi ‘stili’ tunasagika na vumbi la taifa la Bongo, achana na vumbi la Congo. Tuko poa kwa upoa ule wa kupata pumzi ya Saa Godi bila malipo wala bando.

Kuhusu mkwanja bado kitendawili, tena kisichoteguka. Gamba hili gumu ‘laifu’ bado haijageuka! enewei letsi fogeti abauti thozi thingsi kozi ze moo amu tokingi abauti... ze moo ama luzingi mai tempa. Wana, ishu ya pisi kali za kitaa kudeti na madingi mnaichukuliaje? Miaka ya sasa siyo majabu tena. Vidingi vinajibebea tu bebezi zetu laivu bila chenga wala soni. Siku hizi kawaida sana habari hizo, watu  hawashangai tena.

Kila siku pisi kali zinapangiwa mijengo mikali Sinzani, Mikocheni na ushuani kote kwenye ‘apatimenti’ za mamilioni. Vinapakiwa kwenye ndiga za vidingilai kuelekea ‘faivu stazk hotelizi’ kutafuna bata, tena hata uso wa aibu havina. Lipsi zao nyepesi kuviita vidingi ‘switi’, switi? Kidingi kizee kuliko mshua wako unakiita switi? Aibu iliyoje! Mwanzo miye nilidhani labda ishu hizi zipo mabushi tu, kumbe siyo. Tena kwa tauni ogopa sana pisi za kuuza nyago kideoni na Insta.

Najiuliza kweli ni ‘rili lavu’ inayowapushi kwa hivyo vibabu? Ama kuna ‘samusingi bihaindi ze sini’? kwa ‘rili lavu’ nakataa. Ndiyo nakataa, nakataa, najua mtasema naleta pigo za ‘kilongi taimu’. Jiulizeni hizi pisi zinafuata nini kwa vizee? Mbona hatujawahi waona wakitoka na vidingi vilala hoi? Ni njaa na tamaa ndiyo inawapeleka. Havina lolote! laifu tamu na kupushi ndinga kali mjini, ‘lesi wigsi na hai hilizi’ ndiyo msingi wa mapenzi yao. Kwao pesa mbele umri kitu gani bana!

Vina sura nzuri lakini matendo yao mh! temea mate chini. Mtoto wa miaka 22 kutoka na kidingi kinachoitafuta 60 kama siyo laana ni nini? Tena pale sababu ya mapenzi inapokuwa pesa. Vina tamaa na haraka ya maisha mazuri. Kumvulia nguo mtu sawa na babu yako kweli? Siyo kama nazitukana pisi kali. Kwani nyinyi hamzioni? Kutwa kwenye makumbi za burudani na vibabu vyao. Huona sifa hata kudiriki kuwatambulisha katika media. Ujinga mtupu!

Kuna kitu kinanichekesha sana kuhusu hizi pisi. Zikitokewa na vibabu vilofa lofa, utasikia: “Ujana alikula na nani uzeeni ndiyo aje kula na mie?” Lakini kwa vibabu vya kizungu utasikia: “Umri ni namba tu niacheni.” Njaa hizi! Kwao mwenye hela siyo babu ila lofa ndiyo babu. Aibu! hii yote ni kutokana na uvivu wa kufikiri. Vibinti vingi tauni vivivu kufikiri,  ndiyo maana ‘fyucha’ yao ipo kwa wanaume tu. Huamini pesa za wanaume zipo kwa ajili yao.

Wanasahau kabisa kupiga mishe halali. Baadaye utavisikia vikisema “Haki sawa”. Upuuzi mtupu. Nani wa kuitoa hiyo haki kama hali yenyewe iko hivi. Acheni ndoto za Abunuasi nyie! Shughulisheni Bongo siyo mpaka kujiuza kwa hivi vidingi. Kuna kapuuzi kitasema: “Hana lolote wivu tu unamsumbua.” Nikuonee wivu kwani nikikutaka sikupati? Wewe demu wa gari na simu? Mimi naamsha akili zenu zilizolala usingizi wa pono. Maisha ya kijitegesha kwa vibabu vya ‘Westeni Kantri’ acheni.

Huu mwezi wa ‘Valentaini Dei’. Tunataka kuwaona kwenye bata na vibabu hivyo, ukipenda pesa penda na muonekano wake basi. Siyo mnavichuna vidingi na kujibebesha magonjwa, kisha mnakula bata na vijana na kawaambukiza ‘yutiai’ sugu. Pisi za mjini zinapenda kufupisha njia za kupata pesa kwa ujasiriamwili. Na hiyo ndiyo sababu ya tajiri mmoja kumiliki pisi zaidi ya ishirini. Na zinajuana zinapeana zamu kama manesi kwa sababu ya akili ndogo ya kutojishughulisha. Hawanaga akili kabisa.

Valentaini hiyo hapa, Manara na Zaylissa, kule Dulla Makabila na Rushayna. Kuna Diamondi na Zuchu na Harmonize kando ya Poshi Queen. Hii inaweza kuwa ndiyo Valentaini Dei bora kwa “kontenti’ nyingi za mitandaoni.  Kama vipi tukutane next week, coz my love from Cape Verde calling me. Wacha nijiandae na bata la Valentine Day. U feel me? Iwe Valentine ya kujenga upendo zaidi kwa wapendanao. Ila mabwege siku kama hii hugeuka kuwa mwisho wa safari ya penzi lao.

(Picha zilizotumika kwa msaada wa Akili Bandia)