Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tanesco ukataji huu wa miti mitaani mnatukosea

Tanesco ukataji huu wa miti mitaani mnatukosea

Muktasari:

Hongera kwa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), kwa kazi nzuri mnayofanya.

Mhariri,

Hongera kwa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), kwa kazi nzuri mnayofanya.

Ingawa bado mnatakiwa kuongeza juhudi, kwani katika baadhi ya maeneo upatikanaji wa umeme ni changamoto ya kudumu, huku wengine wakilalamika kukatikakatika kila mara.

Mbali na hayo, mnafanya kazi nzuri. Nimejitokeza kuandika barua hii leo kulalamikia mnachokifanya mitaani. Mnapokata miti bila kuwahusisha wamiliki wake bila kujali ni ya matunda au kivuli.

Kuna ambayo kweli ipo mahali ambako inahatarisha usalama wa miundombinu ya umeme, lakini kwingine mnakata tu kwa sababu mna msumeno.

Hii si sawa, hususan mnapokata miti ya matunda ambayo wahusika wametumia nguvu nyingi kuiotesha.

Gabriel Ngaiza, DSM