Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kocha Liverpool amfuta kazi mwamuzi England

Muktasari:

  • Coote alisimamishwa kazi Novemba 11 kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikidaiwa kumuonyesha akitoa matamshi ya dharau dhidi ya Liverpool na kocha wake wa zamani Jürgen Klopp.

London, England. Mwamuzi wa Ligi Kuu ya England, David Coote (42), amefutwa kazi rasmi na shirika la waamuzi wa soka, PGMOL (Professional Game Match Officials Limited), baada ya uchunguzi wa kina kuhusu mwenendo wake wa hivi karibuni.

Coote alisimamishwa kazi Novemba 11, kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikidaiwa kumuonyesha akitoa matamshi ya dharau dhidi ya Liverpool na kocha wake wa zamani Jürgen Klopp, video hiyo ilisababisha mjadala mkubwa huku baadhi ya mashabiki na wachambuzi wa mchezo huo wakionyesha kutoridhishwa na tabia ya mwamuzi huyo.

Tuhuma dhidi ya refa huyu ziliongezeka baada ya gazeti la The Sun kuchapisha picha zinazodaiwa kumuonyesha akitumia dawa za kulevya aina ya cocaine, hatua iliyosababisha afanyiwe uchunguzi zaidi na shirika la waamuzi PGMOL.

David Coote, amechezesha michezo 493 katika mashindano yote huku akifanya hivyo mara 112 kwenye Ligi Kuu England, kwenye ligi daraja la kwanza England amechezesha michezo 143 huku akiwa ametoa kadi za njano 1,762 wakati kadi nyekundu ametoa 117 katika mashindano yote aliyochezesha.

Mwamuzi huyo alianza kuchezesha mchezo wake wa kwanza Aprili 2018 kwenye mchezo kati ya West Brom ambayo ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Newcastle wakati mchezo wa mwisho alichezesha mechi kati ya Liverpool iliyopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Aston Villa Novemba 9, 2024.


Michezo aliyochezesha hivi karibuni:

Nov 9, 2024        Liverpool 2-0 Aston Villa

Oct 27, 2024       West Ham 2-1 Man Utd 

Oct 6, 2024         Brighton 3-2 Spurs           

Sep 21, 2024       Crystal Palace 0-0 Man Utd          

Aug 31, 2024      Leicester 1-2 Aston Villa

Aug 25, 2024      Bournemouth 1-1 Newcastle       

Aug 16, 2024      Coventry 3-2 Oxford Utd              

Aug 13, 2024      Grimsby Town    1-1 Bradford      

May 4, 2024        Arsenal  3-0 Bournemouth            

Apr 27, 2024       Wolves  2-1 Luton            

Apr 14, 2024       Arsenal  0-2 Aston Villa   

Mar 31, 2024      Liverpool 2-1 Brighton   

Mar 3, 2024        Burnley 0-2 Bournemouth            

Feb 28, 2024       Chelsea 3-2 Leeds            

Feb 18, 2024       Luton     1-2 Man Utd      

Feb 10, 2024       Ipswich 2-2 West Brom  

Jan 31, 2024       Spurs     3-2 Brentford    

Jan 28, 2024       Newport 2-4 Man Utd    

Jan 14, 2024       Everton 0-0 Aston Villa   

Jan 10, 2024       Liverpool 2-1Fulham