Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ujenzi wa uhusiano muhimu kati ya maji safi na huduma za kijamii nchini

Miradi ya dharura ya Majisafi, Usafi wa Mazingira na Usafi Binafsi (WASH) inayofadhiliwa na UNICEF katika Wilaya ya Biharamulo wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg iliimarisha upati­kanaji wa maji salama na huduma za usafi katika jamii na vituo vya afya; kusaidia kulinda watoto, familia, na wahudumu wa afya wakati ambapo upatikanaji wa maji safi ulikuwa jambo la muhimu zaidi. (© UNICEF Tanzania /2024).

Upatikanaji wa maji safi ni msingi wa huduma bora za jamii, ukifanya kazi kama kichocheo cha maboresho katika sekta za elimu, afya, na mazingira kote nchini.

UNICEF, kwa kushirikiana na Serikali, inaleta mabadiliko katika sekta hizi kwa kutekele­za miradi ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (WASH) inayo­stahimili mabadiliko ya tabi­anchi, ambayo inalinda utu wa watoto na kuhakikisha mwen­delezo wa huduma muhimu za jamii.


Usambazaji maji shuleni: Kulinda utu na ujifunzaji

Katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, Songwe, na Kigoma pamoja na kule visi­wani Zanzibar, huduma bora za maji na usafi wa mazingira shuleni zinaimarisha afya, utu, na ushiriki kamilifu wa watoto kwenye masomo.

Miundombinu ya uhakika husaidia kupunguza utoro na kuhakikisha mazingira salama na rafiki ya kujifunzia hususan kwa wasichana, ambao wana­hitaji faragha na vifaa salama vya usafi ili kujistiri kwa kuji­amini na amani hususan waka­ti wa hedhi.

Katika shule nyingi, ukosefu wa maji ya uhakika ulisababi­sha watoto kuhangaika kupata maji salama ya kunywa, kuna­wa mikono, au kusafisha miili yao wakati wa masomo.

Kwa wasichana, ilikuwa tofauti, kutokana na usafi duni walilazimika kukosa vip­indi vya masomo kila mwezi hususan pale wanapokua kati­ka hedhi, jambo ambalo lilid­hoofisha maendeleo yao ya kitaaluma na kuongeza pengo la usawa dhidi ya wavulana.

UNICEF, kwa kushirikiana na Serikali na washirika wengine, imesaidia juhudi za kusogeza maji safi karibu na shule kwa kujenga na kukarabati miun­dombinu ya maji safi na mazin­gira inayohimili mabadiliko ya tabianchi na rafiki kwa watoto.

Miundombinu hii ni salama kwa watoto na ina uwezo wa kuhimili changamoto za hali ya hewa kama vile ukame wa muda mrefu au mafuriko.

Uwekezaji huu unakamilish­wa na programu za mabadi­liko ya tabia shuleni ambazo huwashirikisha watoto katika kujifunza na kushiriki katika shughuli za usafi na kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Maarifa haya yanazigu­sa mpaka jamii zao, amba­po watoto wanageuka kuwa mawakala wa mabadiliko.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, huduma na miundombinu bora ya majisafi na usafi wa mazingira imean­zishwa au kukarabatiwa katika zaidi ya shule 110 kote Tanza­nia, ikiwafikia zaidi ya wana­funzi 92,000, wakiwemo wasi­chana 48,000.

Mchanganyiko huu wa pro­gramu za kubadilisha tabia zinazoendeshwa mashuleni na ujenzi wa miundombinu, una­saidia kuweka mazingira ya kujifunzia yaliyo salama, yenye afya na jumuishi zaidi.

Upatikanaji wa maji salama kwa wasichana balehe, vyoo vya faragha, na maeneo safi ya kujistiri wakati wa hed­hi, unawahakikishia fursa ya kuhudhuria masomo kwa kujiamini na heshima. Hiiinathibitisha kuwa maji yanap­opatikana shuleni, usawa wa kijinsia nao hustawi.


Paneli ya umeme wa jua inayoendesha mfumo wa maji wa jamii katika Mkoa wa Kigoma inapanua huduma za maji zinazohimili mabadiliko ya tabianchi. Huduma hizi zinasogeza maji salama karibu na familia na kuwaondolea wanawake na watoto adha ya kutembea umbali mrefu (© UNICEF Tanzania /2026/Magari)/2024/Studio 19).

Usambazaji maji katika vituo vya afya: Kulinda akina mama na watoto wachanga

Upatikanaji wa maji wa uhakika ni hitaji la lazima kwa huduma za afya salama na zenye ubora wa hali ya juu. Bila maji, wahudumu wa afya hawawezi kunawa mikono yao, kusafisha vifaa vya matibabu, au kudumisha viwango vya usafi vinavyohitajika ili kusaid­ia uzazi salama na kutibu wag­onjwa. Hali hii inawaweka aki­na mama, watoto wachanga na jamii nzima katika hatari ya maambukizi ya magonjwa yan­ayozuilika.

Sabrina, mama kutoka kijiji cha Sasama mkoani Songwe, anasimulia alivyokuwa na hofu kujifungulia katika kituo chake cha afya cha karibu kutokana na ukosefu wa maji na usafi.

“Nilikuwa nasita kujifun­gulia hapa kituoni kutokana na matatizo haya yote ya maji na usafi wa mazingira. Sikuta­ka kuhatarisha afya yangu au ya mtoto wangu. Lakini kujif­ungulia nyumbani bila mkun­ga mwenye ujuzi kulikuwa na hatari vile vile,” anasema Sabrina.

Hii ndiyo sababu ni muhimu zaidi kuimarisha huduma kati­ka vituo vya afya ili kuboresha udhibiti wa maambukizi na kuhakikisha huduma salama kwa akina mama na watoto wachanga.

Katika mikoa ya Songwe, Mbeya, na Kagera, UNICEF imesaidia kuboresha miun­dombinu ya majisafi na usa­fi wa mazingira inayohimili mabadiliko ya tabianchi na mifumo ya udhibiti wa taka za afya, hali inayoongeza ubo­ra wa huduma na kunufaisha zaidi ya watu 100,000, ikiwa ni pamoja na idadi kubwa ya wanawake na watoto.

Vituo hivi sasa vina upa­tikanaji wa maji wa uhakika, vyoo vilivyoboreshwa, sehemu salama za kunawia mikono, huduma za kufulia, na mifumo sahihi ya udhibiti wa taka.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, programu zinazofadhiliwa na UNICEF zimeimarisha huduma hizi katika vituo vya afya zaidi ya 90 kote nchini, zikiwanufaisha akina mama, watoto wachan­ga, wahudumu wa afya, na wagonjwa zaidi ya 300,000 kwa ujumla.

Maboresho haya yanapun­guza maambukizi, yakimlinda mama wakati wa kujifungua na kuhakikisha mtoto mchanga anaanza maisha katika mazin­gira safi na salama.


Usambazaji maji wakati wa dharura: Kulinda watoto wakati wa uhitaji mkubwa

Wakati wa dharura, upati­kanaji wa maji safi na salama ni jambo lisilohitaji mjadala. Iwe ni kukabiliana na milipu­ko ya magonjwa, mafuriko, au majanga ya asili, huduma za uhakika za majisafi na usafi wa mazingira hulinda watoto na jamii dhidi ya maambukizi na changamoto nyingine za kimaisha.

Wakati wa mlipuko wa viru­si vya Marburg mkoani Kagera, UNICEF ikifanya kazi kwa kari­bu na Serikali kwa kushiriki­ana na wadau wengine, ilite­keleza mpango wa dharura katika Wilaya ya Biharamulo. Mpango huo ulisaidia kubore­sha upatikanaji wa maji katika Hospitali ya Wilaya ya Bihara­mulo, ambayo ilitumika kama Kituo Kikuu cha Matibabu ya ugonjwa wa Marburg.

Mpango huo ulihusisha uchimbaji wa kisima kipya, ujenzi wa tanki kubwa la maji la lita 50,000, ujenzi wa kituo cha pampu, na uunganishaji maji kwenye majengo ya hos­pitali ili kuhakikisha huduma ya saa 24 inakuwepo bila kuka­tika.

Aidha, katika kijiji cha Kat­erela, ambacho kilikuwa kito­vu cha ugonjwa huo, UNICEF ilisaidia ufungaji wa mfumo wa nishati ya jua, ujenzi wa tanki lingine la lita 50,000, na kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati ya maji ya jamii ili kuhakikisha uendelevu wa huduma hizo. Hatua hizi za dharura za mpango wa maji safi na usafi wa mazingira zili­wafikia zaidi ya watu 400,000, wakiwemo watoto zaidi ya 220,000.

Vilevile, juhudi hizi ni muhimu zaidi katika kambi za wakimbizi na maeneo yali­yoathiriwa na majanga ya asili kama maporomoko ya ardhi wilayani Hanang na mafuriko kule Rufiji.

Katika maeneo haya, maji safi na usafi wa mazingi­ra huzuia magonjwa kama kuhara na kipindupindu. Hata baada ya kadhia hizo kupita, uwekezaji huu unaendelea kuhudumia jamii, kusaidia watoto waendelee kubaki sala­ma na wastahimilivu.

Paneli ya umeme wa jua inayoendesha mfumo wa maji wa jamii katika Mkoa wa Kigoma inapanua huduma za maji zinazohimili mabadiliko ya tabianchi. Huduma hizi zinasogeza maji salama karibu na familia na kuwaondolea wanawake na watoto adha ya kutembea umbali mrefu (© UNICEF Tanzania /2026/Magari)/2024/Studio 19).


Huduma himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi: Kuandaa watoto kwa ajili ya kesho bora ya upatikanaji wa maji

Mabadiliko ya tabianchi tayari yanabadilisha maisha ya watoto nchini kupitia uhaba wa maji, mafuriko, na milipu­ko ya magonjwa. UNICEF ina­fanya kazi kwa kushirikiana na Serikali kujenga mifumo thabiti inayolinda ustawi wa watoto na kuhakikisha mwen­delezo wa masomo na huduma za afya.

Hii ni pamoja na kuimari­sha miundombinu, kukuza shughuli za uhifadhi wa maji kama upandaji miti, na kuwapa vijana ujuzi wa kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Huko Zanzibar, UNICEF inashirikiana na Serikali kuim­arisha ushiriki wa vijana katika miradi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi katika shule za sekondari 216 katika wilaya zote 11 za Unguja na Pemba.

Uwekezaji huu unajumui­sha ujenzi wa vyoo 23 vyenye matundu 190 na mifumo ya maji ya uhakika katika shule 13 kule Pemba. Kupitia klabu za maji safi na usafi wa mazin­gira mashuleni zijulikanazo kama ‘SWASH Club’, wanafun­zi wanajifunza kuwa mabalozi wa uhifadhi wa maji na usafi. Vilabu hivi vinawawezesha watoto kubadili tabia zao na kuwahimiza wazazi wao kulin­da vyanzo vya maji. Mbali na hilo, UNICEF inasaidia vijana kushiriki katika mijadala ya kitaifa na kimataifa ya tabian­chi ili sauti zao ziweze kuleta masuluhisho ya siku za usoni.


Uimarishaji mifumo: Msingi wa maji endelevu na usawa

Nyuma ya kila kituo cha maji kinachofanya kazi, choo sala­ma cha shule, au sehemu ya kunawia mikono katika kituo cha afya, kuna mfumo imara, unaowajibika, na wenye rasili­mali za kutosha. Tanzania imepiga hatua kubwa katika kupanua upatikanaji wa maji safi; kulingana na Mpango wa Pamoja wa Ufuatiliaji wa WHO/UNICEF (JMP), idadi ya watu wanaotumia huduma za msingi za maji iliongezeka kutoka asilimia 50 mwaka 2015 hadi asilimia 64 mwaka 2024.

Hata hivyo, kudumisha mafanikio haya kunahitaji sera madhubuti, taasisi zenye uwezo, na mifumo imara ya ufuatiliaji.

UNICEF inasaidia juhudi za Serikali katika kuimari­sha mifumo ya kitaifa na ya mikoani kwa ajili ya kupanga bajeti na kusimamia uwaji­bikaji. Mifumo ya ufuatiliaji inaboreshwa kupitia majuk­waa ya kidijitali na miongo­zo ya takwimu ili kuhakikisha huduma zinadumu muda mre­fu baada ya miradi kukamilika.

Vilevile, UNICEF inasaidia hatua za kisekta kuhusu mahi­taji ya wasichana balehe kupi­tia miongozo ya kitaifa ya hed­hi salama pamoja na nyenzo zake za kuetendea kazi. Juhu­di hizi za kimfumo ni muhimu kwa sababu maji na usawa wa kijinsia haviwezi kutenganish­wa.

Ukosefu wa usawa wa kim­fumo huamua nani anapata huduma, nani anapata kwa uchache, na nani anashiriki katika kufanya maamuzi. Kwa kuimarisha mifumo na kuju­muisha viwango vinavyozin­gatia jinsia, UNICEF inahaki­kisha maendeleo yanawafikia wale walioachwa nyuma zaidi, hususan wasichana.

Paneli ya umeme wa jua inayoendesha mfumo wa maji wa jamii katika Mkoa wa Kigoma inapanua huduma za maji zinazohimili mabadiliko ya tabianchi. Huduma hizi zinasogeza maji salama karibu na familia na kuwaondolea wanawake na watoto adha ya kutembea umbali mrefu (© UNICEF Tanzania /2026/Magari)/2024/Studio 19).


Ushirikiano: Kufanya kazi pamoja kwa huduma za maji endelevu

Kupanua upatikanaji wa maji safi nchini kunahitaji ush­irikiano thabiti na wa kudumu. Maendeleo ya dhati yanat­egemea hatua zilizoratibiwa na uwekezaji wa muda mrefu kutoka kwa Serikali, washirika wa maendeleo na jamii.

UNICEF inafanya kazi kwa karibu na wizara mbalimba­li kama vile Wizara ya Maji, Wakala wa maji vijijini - RUWASA, Wizara ya Afya, Wiz­ara ya Elimu, na TAMISEMI. Kule Zanzibar, inashirikiana na Wizara ya Maji, Nishati na Madini (MoWEM) na Mamla­ka ya Maji Zanzibar (ZAWA). Ushirikiano huu unahakikisha umiliki wa kitaifa wa miradi ya maji na kuimarisha utekelezaji wa sera ili huduma ziwafikie watoto walio hatarini zaidi.

Juhudi hizi zinawezekana kupitia msaada wa wahisani kama Serikali za Uholanzi, Japan, Ireland, Norway, Jam­huri ya Korea, na mashirika kama Grundfos Foundation, Education Above All, Qatar Fund for Development, na CDC ya Marekani. Pia, UNICEF inashirikiana na asasi za kiraia kama Water Mission, Red Cross Tanzania, na nyinginezo ambazo uwepo wao katika jamii unahakikisha masu­luhisho ya maji yanadumu. Katika kipindi cha miaka mita­no iliyopita, zaidi ya watoto na familia milioni 7.5 wamefikiwa na huduma za majisafi na usafi wa mazingira.


Hitimisho: Kesho yenye usawa wa kijinsia unaokua kwa kasi

Maji yanapotiririka kari­bu na nyumbani, maisha yanabadilika. Msichana anafi­ka shuleni kwa wakati bada­la ya kutembea umbali mre­fu. Mama anajifungua katika kituo safi na salama. Familia zinakunywa maji salama, zin­afanya usafi, na zinajiweka mbali na magonjwa ya maam­bukizi. Jamii zinaimarika zaidi pale ambapo muda, usalama, na fursa vinarudishwa kwa wanawake na wasichana.

Lakini usawa wa kweli una­hitaji zaidi ya upatikanaji wa uhakika wa maji salama. Ina­hitaji kuhakikisha kuwa wan­awake na wasichana siyo tu wapokeaji wa huduma za maji, bali ni washiriki hai katika kuz­ianzisha.

Wanawake na wasichana wanaposhirikishwa kikamili­fu katika kupanga, kufanya maamuzi, na usimamizi wa maji, masuluhisho yanakidhi mahitaji ya watu vizuri zaidi, yanakuwa endelevu, na yenye usawa zaidi.

Kwa sababu, mahali amba­po maji yanatiririka, na mahali ambapo wanawake na wasi­chana wanapewa fursa ya kuongoza, usawa wa kijinsia hustawi.