Dk Tulia awapa matumaini ya ushindi CCM, aahidi ujenzi wa soko la kisasa Nsalaga
Muktasari:
- Kauli hiyo ameitoa leo Jumatatu Septemba 22,2025 wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Itezi Kata ya Nsalaga Jijini Mbeya.
Mbeya. Mgombea ubunge Uyole Mkoa wa Mbeya, Dk Tulia Ackson amesema wakati wa hesabu kura za Chama cha Mapinduzi (CCM), umefika na kutaja kipaumbele ni ujenzi wa soko la kisasa la Nsalaga ili kuchochea shughuli za kiuchumi kwa wajasiriamali.
Mbali na uwekezaji wa Soko, pia amesema Serikali imeweza kutekeleza ilani ya uchaguzi 2020/25 kwa kuondoa hadha ya watoto kukaa chini katika shule za msingi na Sekondari kwenye Mbeya Mjini na Uyole kabla halijatangazwa kuwa Jimbo jipya.
Hatua hiyo imetajwa ni kupunguza mzigo kwa wananchi na wazazi kuchangia elimu na shughuli za kiuchumi.
Dk Tulia amesema jana Jumatatu Septemba 22, 2025 katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Itezi Kata ya Nsalaga.
"Umefika wakati wa CCM kuhesabu kura na kusema yaliyo fanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika sekta mbalimbali za elimu, afya na maji na barabara katika kupiga hatua za maendeleo," amesema.
Amesema awali kabla ya Serikali kugawanya Jimbo jipya la Uyole aliweza kutumikia kata 36 hizi 13 zilizobaki atazicharaza kwa kuleta maendeleo.
Katika hatua nyingine, Dk Tulia amesema binafsi amemshukuru Rais Samia kwa kuridhia kuanzisha Jimbo jipya la Uyole na kuwaondoa hofu wananchi maendeleo yataletwa kwa kasi.
Amesema ilani ya uchaguzi 2020/ 2025 mpaka 2030 imeelekeza kila kata zenye idadi kubwa ya watu kujengwa vituo vya afya lengo ni kusogeza huduma bora kwa jamii.
"Jamani mambo makubwa yanakuja kazi yenu ni kumpa kura za kishindo mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Oktoba 29,2025, amesema ," amesema.
Sambamba na hilo amesema ataendelea kuboresha utoaji wa bima za afya kwa wananchi wenye uhitaji .