Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wanawake 100,000 kunufaika na mafunzo ya teknolojia za kidijitali nchini

Mkurugenzi wa Jinsia katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Badru Abdunuru (katikati), akishuhudia utiaji saini wa makubaliano ya kuimarisha sekta ya uvumbuzi wa kidijitali kwa wanawake. Kulia ni Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la GIZ, Anne Hahn, na kushoto ni Kaimu Mkuu wa Ushirikiano katika Ubalozi wa Ujerumani, Marlene Landes. Picha na Said Powa.

Muktasari:

  • Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) zasaini makubaliano ya utekelezaji kuimarisha ushirikishwaji wa wanawake katika teknolojia za kidijitali na uwezeshaji wa kiuchumi.

Dar es Salaam. Wanawake na wasichana zaidi ya 100,000 nchini wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kiteknolojia za kidijitali yatakayowawezesha kupata fursa ya kutumia vifaa vya kisasa vya kidijitali, teknolojia zinazoibuka, kushiriki katika ubunifu wa vitendo na kujengewa stadi za kisasa zinazohitajika katika uchumi wa kidijitali.

Mafunzo hayo watayapata katika Kituo cha Ubunifu na Utengenezaji Teknolojia kitakachokuwepo katika Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO), ambapo wanawake na wasichana watahama kutoka kuwa watumiaji wa teknolojia pekee na kuwa wabunifu, wavumbuzi na wajasiriamali wa teknolojia katika uzalishaji mali na bunifu mbalimbali.

Hilo linafutatia hatua ya Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Ujerumani (GIZ) kusaini Makubaliano ya Utekelezaji wa Mradi wa Kituo cha Mabadiliko ya Kidijitali Tanzania DTC, ikiwa ni hatua kuendeleza matumizi ya teknolojia za kidijitali katika kukuza usawa wa kijinsia na mabadiliko ya kidijitali yanayomjumuisha kila mwananchi nchini.

Kupitia makubaliano hayo ya miaka mitatu yanalenga kuimarisha matumizi ya mbinu za kidijitali katika kukabiliana na changamoto za kijamii na kiuchumi, sambamba na kuhakikisha wanawake na wasichana wanashiriki kikamilifu na kunufaika na ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.

Akizungumza Alhamisi, Juni 11, 2026 jijini Dar es Salaam katika halfa ya utiaji saini, Mkurugenzi wa Jinsia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Badru Abdunuru amesema lengo ni kuwafikia wanawake 100,000 kupitia mradi huo wa miaka mitatu ya awali ingawa inaweza kufikiwa wanawake wengi zaidi.

“Mradi unataka kuimarisha ushiriki wa wanawake na wasichana kwenye uchumi wa kidijitali ili kuongeza ushiriki wao kupitia mafunzo mahususi yatakayopatikana Shirika la TIRDO ya namna ya kutumia teknolojia hizo,” amesema.

Amesema kituo hicho kitakuwa na zana zote za kujifunzia namna ya kutumia teknolojia katika uzalishaji wao na mafunzo pia yatapatikana katika vituo vya chuo cha maendeleo ya jamii, na Tengeru.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi mkaazi wa GIZ Tanzania, Anne Hahn amesema ushirikiano huu tayari ulishaanza kuzaa matunda kabla hata ya utiaji saini wa makubaliano rasmi.

“Kupitia ushirikiano na Shirika la TIRDO, GIZ inasaidia kuanzisha maabara ya kidijitali na karakana ya ubunifu maalum kwa ajili ya wanawake na wasichana ili kuwageuza kuwa wabunifu na wajasiriamali,’’ amesema.

Marlene Landes, Kaimu Mkuu wa Ushirikiano ubalozi wa Ujerumani amesema utiaji saini unaonyesha nia ya pamoja ya kuhakikisha mabadiliko ya kidijitali yanatoa fursa kwa kila mtu bila kuacha mtu nyuma.

Amesema teknolojia inapaswa kutumika kwa uwajibikaji ili kukuza uhuru wa kujieleza, kupata taarifa, na uwezeshaji wa kiuchumi.

Kwa upande wake Mhandisi Esther Lazaro kutoka TIRDO, amesema kupitia mradi huo wanawake na wasichana watageuza mawazo yao kuwa bidhaa kupitia msaada wa kidijitali utakaotolewa na kituo hicho.

“Tutafanya watatue matatizo yanayowakabili wanawake na Tanzania kwa ujumla kupitia vifaa na mafunzo watakayoyapata,” amesema.

Mradi    huo unaendana na vipaumbele vya maendeleo vya taifa vilivyobainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Jinsia na Wanawake ya Mwaka 2023, Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto pamoja na Mkakati wa Uchumi wa Kidijitali wa Mwaka 2024–2034.

Aidha, GIZ kwa kushirikiana na Tanzania inaendelea na maandalizi ya kuanzisha Maabara ya Ubunifu wa Kidijitali (Digital Fabrication Lab).


// Block all Eskimi ads (function () { const keyword = 'eskimi'; // 1. Intercept JSON/String payloads globally (Crucial for SafeFrame data) // Google passes ad payloads as serialized strings. We intercept JSON parsing. const originalParse = JSON.parse; console.error(originalParse); JSON.parse = function (text) { if (typeof text === 'string' && text.toLowerCase().includes(keyword)) { console.warn(`[Aggressive Block] Corrupted an Eskimi JSON payload.`); // Return empty or modified data to force the ad creative to crash safely return {}; } return originalParse.apply(this, arguments); }; // 2. Intercept PostMessage (How SafeFrames communicate with your page) // SafeFrames constantly talk to the host page via postMessage. We block Eskimi messages. const originalPostMessage = window.postMessage; window.postMessage = function (message, targetOrigin, transfer) { try { const serialized = typeof message === 'string' ? message : JSON.stringify(message); if (serialized.toLowerCase().includes(keyword)) { console.warn(`[Aggressive Block] Dropped Eskimi postMessage.`); return; // Kill the communication line } } catch (e) {} return originalPostMessage.apply(this, arguments); }; // 3. Google Publisher Tag (GPT) Inception window.googletag = window.googletag || { cmd: [] }; window.googletag.cmd.push(function() { // Intercept slot rendering before it hits the DOM window.googletag.pubads().addEventListener('slotRenderEnded', function(event) { const elementId = event.slot.getSlotElementId(); const container = document.getElementById(elementId); if (!container) return; // Attack 1: Scan attributes & hidden configuration scripts inside the container const innerHTML = container.innerHTML.toLowerCase(); if (innerHTML.includes(keyword)) { nukeContainer(container, elementId, 'Found in HTML/Scripts'); return; } // Attack 2: Force-inspect the Iframe's name/title configurations const iframes = container.querySelectorAll('iframe'); iframes.forEach(iframe => { const identifier = [ iframe.id, iframe.name, iframe.getAttribute('title'), iframe.getAttribute('data-google-container-id') ].join(' ').toLowerCase(); if (identifier.includes(keyword)) { nukeContainer(container, elementId, 'Found in Iframe attributes'); } }); }); }); function nukeContainer(container, id, reason) { console.warn(`[Aggressive Block] Nuking slot ${id}. Reason: ${reason}`); container.innerHTML = ''; // Wipe out the iframe completely container.style.setProperty('display', 'none', 'important'); // Collapse the layout container.style.setProperty('visibility', 'hidden', 'important'); container.style.setProperty('height', '0px', 'important'); } // 4. Extreme DOM Reaper (Runs every 400ms to catch lazy loads) setInterval(() => { // Target all standard Google ad wrappers and SafeFrame wrappers const targets = document.querySelectorAll('.ad-medium-rectangle, [id^="google_ads_iframe"], [id^="gpt_ad"], iframe[src*="safeframe"]'); targets.forEach(el => { // Check outer HTML for serialized config strings (Google leaves queries in data attributes) const outer = el.outerHTML.toLowerCase(); if (outer.includes(keyword)) { const parentSlot = el.closest('.ad-medium-rectangle') || el; nukeContainer(parentSlot, parentSlot.id || 'Unknown Slot', 'Reaper detected keyword'); } }); }, 400); })();