Lowassa: Njia ya Ikulu 2020 nyeupe

Muktasari:

“Kuweni watulivu  na mwaka 2020 mjitokeze kupiga kura na kama nitakuwa  hai nitakuwa mgombea tena wa urais kupitia muungano wa vyama vya upinzani,” alisema.

Kahama. Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa amesema njia ni  nyeupe kwa Chadema kuingia Ikulu katika uchaguzi ujao wa mwaka 2020.


“Kuweni watulivu  na mwaka 2020 mjitokeze kupiga kura na kama nitakuwa  hai nitakuwa mgombea tena wa urais kupitia muungano wa vyama vya upinzani,” alisema.


Akizungumza nyumbani kwa kada wa Chadema, James Lembeli katika kijiji cha  Mseki, Kahama, Lowassa (pichani) alisema ameshindwa kuzungumza na kufanya mkutano na  wananchi wa kijiji hicho akihofia kukamatwa na polisi kama alivyokamatwa Geita na kuwataka wawe wavumilivu hadi uchaguzi wa mwaka 2020.


Kadhalika, Lowassa aliwataka vijana wasikubali kuibiwa kura kwa madai uchaguzi uliopita hawakutendewa haki na ndio maana walikosa ushindi.