JPM aeleza faida uanzishwaji kwa viwanda kila mkoa
Muktasari:
Ametoa kauli hiyo wakati akizindua kiwanda cha sigara cha Philip Moris
Morogoro. Rais John Magufuli amesema uazishwaji wa viwanda katika kila mkoa utasaidia kuondoa kero zilizokuwa zikilalamikiwa wakulima wa tumbaku hasa Mkoa wa Tabora.
Akizungumza leo Machi 15, 2018 katika uzinduzi wa kiwanda cha sigara cha Philip Moris mjini Morogoro, Rais Magufuli amewataka Watanzania kubadilika kwa kuwekeza katika viwanda, kwamba suala la viwanda linawezekana na enzi za Morogoro ya viwanda itawezekana.
“Tusirudie tena kuua viwanda Serikali itaunga mkono viwanda vyote vinavyoanzishwa. Nafahamu kuna baadhi ya vikodi kodi vinavyoleta kero, tayari nimeshatoa maelekezo kwa waziri wa viwanda kuangalia upya hizo kodi,” amesema.
“Wawekezaji tutalinda viwanda msihofu kujenga viwanda. Niwaombe viongozi wenzangu tusiwe vikwazo kwa wawekezaji kuja kuwekeza.”