VIDEO: Maisha mapya ya wafanyakazi Clouds bila Ruge
Muktasari:
Wasema marehemu aliwatengeneza kina Ruge wengi wanaamini baada ya muda watakaa sawa
Dar es Salaam. Ingawa sio wote walioripoti ofisini baada ya kumaliza mazishi siku tatu zilizopita, wachache wameendelea na kazi kama ilivyoshuhudiwa na waandishi wa MCL Digital.
Shaffih Dauda ambaye ni mkurugenzi wa vipindi wa Redio Clouds anasema wanaumia lakini wanaweza kuendelea na maisha kwa kuenzi matendo yake aliyokuwa akipenda yafanyike enzi za uhai wake.
Amesema Ruge hakuwa mchoyo wa maarifa kitu ambacho kimefanya kampuni yao iwe na jeshi kubwa litakaloendeleza aliyopenda.
Naye mtangazaji, Kennedy the Remedy amesema bosi wao amewaachia utajiri mkubwa wa maarifa mfano wa mtu aliyekuwa akiwaandaa kuwa warithi wake atakapoondoka.
“Kama unavyoona bado hatujakaa vizuri lakini kusema ukweli tupo tayari kumuenzi bosi wetu kwa kupiga kazi na kujiamini kama alivyopenda kila mmoja wetu afanye,” amesema Kennedy.