Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Hapa Ommy Dimpoz kachemka pakubwa! 

Muktasari:

  • Hata hivyo, mradi huo uliotoka rasmi Oktoba 28, 2022, hakuwa na matokeo makubwa ukilinganisha na umaarufu wa jina lake na jinsi ambavyo amekuwa akitajwa au kuhusika katika matukio mengi ya kiburudani na mengineo hapa Bongo.

Dar es Salaam. Ni miaka mitatu imepita tangu staa wa Bongofleva, Ommy Dimpoz alipoachia albamu yake ya kwanza, Dedication (2022) chini ya Sony Music na RockStar Africa, huku ikiwa na nyimbo 15 pamoja na kuwashirikisha wasanii 10 wa ndani na nje.

Hata hivyo, mradi huo uliotoka rasmi Oktoba 28, 2022, hakuwa na matokeo makubwa ukilinganisha na umaarufu wa jina lake na jinsi ambavyo amekuwa akitajwa au kuhusika katika matukio mengi ya kiburudani na mengineo hapa Bongo.

Mbali na hilo, tangu alipotoa albamu hiyo ameachia wimbo mmoja pekee, Nitakupa (2024) uliotoka miezi 11 iliyopita na kumshirikisha Jay Melody, mwanamuziki mwenye albamu mbili aliyetoka na kibao chake, Goroka (2018).

Hii ni ishara ya kushuka kimuziki au kutozingatia kama ilivyokuwa awali ambapo alitoa nyimbo kila wakati na pia zikawa maarufu akishinda Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) na zile za kimataifa kama African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA).

Utakumbuka Ommy Dimpoz alianzisha lebo yake, Poz kwa Poz (PKP) Entertainment lakini haikutajwa katika albamu hii na hilo linaacha maswali iwapo imekufa rasmi au aliposaini Sony Music na Rockstar Africa alitakiwa kuiweka pembeni.

Mbali na hilo albamu yake ilitoka kwa kuchelewa sana, yaani ilikuja miaka 10 baada ya yeye kutoka kimuziki wakati wasanii wengi hutoa albamu ndani ya miaka mitatu hadi mitano ya mwanzo ya umaarufu wao.

Katika nyimbo 15 za albamu yake, Dedication (2022), ni mbili pekee ambazo zilitolewa video zake, nyimbo hizo ni ‘Vacation’ uliotoka kabla ya albamu hiyo, na mwingine ni ‘Anaconda’ akilishirikisha kundi la Black Diamond kutokea Afrika Kusini.

Mashabiki wengi walitegemea kolabo yake na Fally Ipupa ‘Mom Bebe’ kutoka ndani ya albamu hiyo ingefanyiwa video lakini hajawa hivyo hadi sasa licha ya ukubwa wa gwiji hiyo kutoka DR Congo aliyeshirikiana na Diamond Platnumz hapo awali.

Kwa mujibu wa Ommy Dimpoz, alikutana na Fally Ipupa Mwanza na wakakubaliana warekodi ila Fally akamwambia inabidi amfuate Paris, Ufaransa ambapo ndipo walirekodiwa na Dimpoz hakumlipa fedha kwa kufanya kolabo hiyo.

Ikumbukwe Dimpoz alitoka kimuziki na kibao chake, Nai Nai (2012) kilichotayarishwa na KTG, kufanya vizuri kwa wimbo huo kulimwezesha kushinda TMA kama Msanii Bora Chipukizi akipokea kijiti kutoka kwa Linah aliyeshinda mwaka 2011.

Huyu ndiye msanii pekee Bongo kushinda TMA mara mbili mfululizo katika kipengele cha Wimbo Bora wa kushirikiana akishinda 2012 na 2013 kupitia ngoma zake ‘Nai Nai’ na ‘Me and You’ alizoshirikiana na Alikiba na Vanessa Mdee.

Baada ya jina lake kuwa kubwa ndipo akaanzisha Poz kwa Poz (PKP) Entertainment, lebo iliyosimamia kazi zake lakini pia ikamsaini Nedy Music aliyetoka kupitia wimbo wake, Usiende Mbali (2016) ambao pia alimshirikisha Dimpoz mwenyewe. 
 
Kwa muda mfupi wimbo huo ukakamata chati za vituo vikubwa vya televisheni kimataifa kama MTV Base, Sound City, Trace Urban n.k, na hadi sasa ni wimbo wa tatu wa Nedy uliofanya zaidi YouTube ukiwa umetazamwa mara milioni 1.7.

Ila kufuatia Dimpoz kusainiwa RockStar Africa (2017) na baadaye Sony Music Entertainment Africa, huo ukawa mwanzo wa Nedy Music kutengwa au kuwa mbali na PKP na hatimaye kuachana nayo kabisa.  

Tetesi za kuachana zilianza alipoachia wimbo, One and Only (2018) akiwa na Ruby, video yake ilitoka bila nembo (logo) ya PKP ndipo maneno yakaanza ila mwaka mmoja kabla Dimpoz alidai kuwa amemtafutia Nedy menejimenti nyingi.

Wimbo huo wa kwanza wa Nedy Music nje ya PKP ulifanya vizuri ukishinda All Africa Music Award (AFRIMA) 2018 katika kipengele cha African Fans Favourite, tuzo zilizofanyika nchini Ghana.

Nedy Music aliyeanza muziki mwaka 2013 akijiunga na Tanzania House of Talent (THT), kushinda tuzo hiyo kulimfanya kuandika rekodi kama mwanamuziki wa kwanza kutokea Zanzibar kushinda AFRIMA.

Tangu Nedy kuachana na PKP ukawa mwanzo wa lebo hiyo kupotea kabisa katika soko la rekodi lebo Bongo na Dimpoz hajawahi kusaini tena msanii mwingine.

Ikumbukwe Ommy Dimpoz alianza safari ya muziki akiwa Sekondari katika kundi lao walilolipa jina la VIP lililoundwa na watu wanne, kisha akaja kujiunga na Top Band yake TID akiungana na waimbaji wengine akiwamo Steve RnB.