Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Askari Mkomazi auawa na nyati

Muktasari:

  • Askari wa Uhifadhi, katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Samwel Edward Nassari amefariki dunia baada ya kugongwa na Nyati katika eneo la Mbula lilipo katika hifadhi hiyo, Wilaya ya Same, Mkoani Kilimanjaro.

Same. Askari wa Uhifadhi, katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Samwel Edward Nassari amefariki dunia baada ya kugongwa na nyati katika eneo la Mbula lilipo katika hifadhi hiyo, wilayani ya Same, Mkoa wa Kilimanjaro.

 Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamishna Msaidizi Hifadhi ya Mkomazi, Emmanuel Moirana amesema tukio hilo limetokea leo Jumanne Agosti Mosi, 2023 wakati askari huyo akitekeleza majukumu yake.

"Mtumishi mwenzetu amefariki leo baada ya kugongwa na nyati wakati akiwa kwenye majukumu yake ya kazi," amesema Moirana

Naye Kamishna wa Uhifadhi Tanapa, William Mwakilema ametuma salamu za pole kwa familia, watumishi wote wa Jeshi la Uhifadhi, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha askari huyo.