Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

H Baba: Ndoa yangu na Florah Mvungi bado ipo

Muktasari:

  • H Baba amejibu tuhuma za ndoa yake kuvunjika ikiwa ni siku moja tangu Florah Mvungi aeleze kwamba wameachana miaka mitatu iliyopita

Dar es Salaam. Nani anasema ukweli? Ndilo swali wanalojiuliza sasa mashabiki wa wanandoa H Baba na Florah Mvungi mmoja akisema wameachana na mwingine anadai hakuna kitu kama hicho.

Florah ambaye ni mwigizaji wa filamu aliyejizolea umaarufu kupitia mchezo wa Bongo Dar es Salaam, aliimbia Mwananchi jana Machi 12, kuwa aliachana na mumewe H Baba miaka mitatu iliyopita lakini hawakutaka kuliweka hilo wazi kwa sababu ambazo alidai ni siri yao.

Mwananchi imezungumza  H Baba ambaye kwa sasa makazi yake yapo mkoani Mwanza na amesema anamtambua Florah kuwa mke wake halali tangu walipofunga ndoa mwaka 2013.

Akizungumza leo Machi 13, 2019, H Baba aliyewahi kutamba na muziki wa aina ya Bongo Bolingo, amesema hawezi kuachana na mkewe kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram au vyombo vya habari kwani ndoa yao walifunga kwa kufuata taratibu zote za dini na kifamilia.

“Siwezi kuachana na mke wangu Instagram, kama nilivyofuata taratibu wakati namuoa ndivyo nitakavyofanya ukifika wakati wa kuachana naye lakini mtambue kwamba Florah bado ni mke wangu na ninampenda sana.

 “Hayo mambo yao ya Bongo Dar es Salaam ya kuzungumzia mpaka masuala ya familia kwenye mitandao huwa siyapendelei na sijalelewa hivyo muulizeni vizuri awaonyeshe talaka,” amesema H Baba aliyewahi kutamba na nyimbo Mpenzi Bubu na Poteza.