Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Hanang kupata mvua za wastani siku mbili mfululizo

TMA yatahadharisha mvua kubwa Dar, Mtwara kimbunga Jobo kikipungua kasi

Muktasari:

  • Mamlaka Hali ya Hewa nchini (TMA), imetoa utabiri unaoonyesha kuwapo kwa mvua za wastani kwa siku mbili mfululizo kuanzia leo wilayani Hanang.

Dar es Salaam. Mamlaka Hali ya Hewa nchini (TMA), imetoa taarifa ya utabiri wa hali ya hewa eneo la Katesh wilayani  Hanang Mkoa wa  Manyara ukionyesha kuwa kutakuwa na mvua za wastani kwa siku mbili mfululizo kuanzia leo.

Akitoa utabiri huo leo Desemba 8, 2023 Meneja Utabiri wa mamlaka hiyo, Dk Mafuru Kantamla amesema kuanzia leo hadi kesho Desemba 9, 2023 mvua za wastani zitanyesha wilayani humo.

Dk Kantamla amesema mvua hizo zinatarajiwa kuanza leo Desemba 8, 2023 saa 12 jioni hadi saa 6 usiku, ambapo zitakuwa za wastani, mawingu kiasi na upepo wa wastani unaofikia kilomita 20 hadi 30 kwa saa, huku joto nyuzi likiwa kati ya 25C na 15C.

Kwa kesho Desemba 9, 2023, Dk Kantamla amesema mvua hizo zitaanza saa 9 alasiri hadi saa 6 usiku, zikiandamana na mawingu kiasi huku upepo ukitarajiwa kuvuma kwa kilomita  20 hadi 30 kwa saa na joto litakuwa kati ya nyuzi joto 25C na 15C.

"Huu utabiri unaonyesha mvua zinazotarajia kunyesha maeneo ya Wilaya ya Hanang, zitakuwa ni za kawaida sana," amesema Dk Kantamla.