Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

JK ateua majina ya wabunge wa bunge la Katiba

Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Florens Turuka

Muktasari:

  • Ni majina ya Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba litakalokaa kwa siku 70 hadi 90 mjini Dodoma kujadili Rasimu ya Katiba Mpya

Dar es Salaam. Hatimaye Rais Jakaya Kikwete amekamilisha uteuzi wa majina ya Wajumbe 201 wa Bunge Maalumu la Katiba, litakaloanza vikao vyake Februari 18 mjini Dodoma.

Kupitia uteuzi huo amewarejesha bungeni wanasiasa wakongwe akiwamo Kingunge Ngombale Mwiru na Paul Kimiti na kuwakumbuka pia wanasiasa wakongwe ambao hawakuwahi kuwa wabunge.

Baadhi ya wanasiasa hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha (NLD) Dk Emmanuel Makaidi na Mwenyekiti wa Chama cha Ustawi Tanzania (Chausta) James Mapalala.

Pia wamo Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila na John Chipaka ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Tadea.

Bunge hilo litajumuisha wabunge wote 357 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wajumbe 82 wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar pamoja na 201 waliotangazwa jana na kufanya idadi yao kuwa 640.

Akitaja majina hayo jana Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Florens Turuka alisema wajumbe hao wameteuliwa kutoka katika makundi 10 ya kijamii.

Aliyataja makundi hayo na idadi ya walioteuliwa katika mabano kuwa ni Taasisi zisizo za Kiserikali (20), Taasisi za Dini (20), Vyama vya Siasa (42), Taasisi za Elimu (20), Makundi ya Walemavu (20), Vyama vya Wafanyakazi (19), Vyama vya Wafugaji (10), Vyama vya Wavuvi (10), Vyama vya Wakulima (20) na Makundi yenye Malengo yanayofanana (20).

“Taasisi 554 kutoka Tanzania Bara na 178 kutoka Zanzibar ziliwasilisha mapendekezo yao yaliyojumuisha majina 2,762 kwa upande wa Bara na upande wa Zanzibar yalihusisha watu 874,” alisema na kuongeza:

“Majina yote yalikuwa 3,636, lakini kinyume na sheria watu 118 walipendekeza wenyewe na kufanya idadi ya majina yaliyopendekezwa kuwa 3,754. Taasisi hizo zilileta majina mengi na kazi ya kuyachuja mpaka kubaki 201 ilikuwa ngumu,” alisema Turuka.

Alisema uteuzi huo umezingatia umri wa waombaji na kwamba wenye umri kuanzia miaka 22 hadi 35 wapo 35, wenye umri wa miaka 36 hadi 60 ni 145 na kuanzia miaka 65 na kuendelea wapo 21.

“Wameteuliwa kwa kuangalia umri, jinsi, uzoefu, sifa na mahali anapotoka mjumbe husika. Wanawake wapo 100 na wanaume wapo 101, wajumbe waliotokea Zanzibar ni 67 na waliotokea Tanzania Bara ni 134,” alisema.

Alisema katika kila kundi wajumbe kutoka Tanzania Bara wapo theluthi mbili na wale kutoka Zanzibar theluthi moja.

Katika kundi la Taasisi zisizokuwa za Kiserikali watu maarufu walioteuliwa ni pamoja na Paul Kimiti, ambaye amewahi kuwa Waziri wa Ajira na Maendeleo ya Vijana na Waziri wa Kilimo na Biashara, kati ya mwaka 1995 na mwaka 2000.

Mbali na Kimiti, pia yupo Kingunge, ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwamo uwaziri katika Serikali za awamu zote nne, tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa upande wa Taasisi za Kidini yupo Profesa Costa Mahalu, Askofu wa Dayosisi ya Kati Kanisa la Mennonite, Amos Muhagachi, Sheikh Mussa Yusuf Kundecha na Sheikh Hamid Masoud Jongo.

Vyama vya Siasa yumo Shamsa Mwangunga ambaye amewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mwenyekiti wa (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.

Majina kamili ya Wajumbe wa Bunge hilo ni :

Tanzania Bara (13)

1. Magdalena Rwebangira

2. Kingunge Ngombale Mwiru

3. Asha D. Mtwangi

4. Maria Sarungi Tsehai

5. Paul Kimiti

6. Valerie N. Msoka

7. Fortunate Moses Kabeja

8. Sixtus Raphael Mapunda

9. Elizabeth Maro Minde

10. Happiness Samson Sengi

11. Evod Herman Mmanda

12. Godfrey Simbeye

13. Mary Paul Daffa

Tanzania Zanzibar(7)

1. Idrissa Kitwana Mustafa

2. Siti Abbas Ali

3. Abdalla Abass Omar

4. Salama Aboud Talib

5. Juma Bakari Alawi

6. Salma Hamoud Said

7. Adila Hilali Vuai

Taasisi za Dini- (Wajumbe20)

Tanzania Bara(13)

1. Tamrina Manzi

2. Olive Damian Luwena

3. Shamim Khan

4. Mchungaji Ernest Kadiva

5. Sheikh Hamid Masoud Jongo

6. Askofu Donald Leo Mtetemela

7. Magdalena Songora

8. Hamisi Ally Togwa

9. Askofu Amos J. Muhagachi

10. Easter Msambazi

11. Mussa Yusuf Kundecha

12. Respa Adam Miguma

13. Profesa Costa Ricky Mahalu

Tanzania Zanzibar(7)

1. Sheikh Thabit Nouman Jongo

2. Suzana Peter Kunambi

3. Sheikh Nassoro Mohammed Ibrahimu

4. Fatma Mohammed Hassan

5. Louis Majaliwa

6. Yasmin Yusufali E. H alloo

7. Thuwein Issa Thuwein

Vyama vyote vya Siasa vyenye Usajili wa  Kudumu– (Wajumbe 42)

Tanzania Bara (28)

1. Hashim Rungwe Spunda

2. Thomas Magnus Mgoli

3. Rashid Hashim Mtuta

4. Shamsa Mwangunga

5. Yusuf S. Manyanga

6. Christopher Mtikila

7. Bertha Ng’angompata

8. Suzan Marwa

9. Dominick Abraham Lyamchai

10. Mbwana Salum Kibanda

11. Peter Kuga Mziray

12. Isaac Manjoba Cheyo

13. Dk Emmanuel John Makaidi

14. Profesa Ibrahim Lipumba

15. Modesta Kizito Ponera

16. Profesa Abdallah Safari

17. Salumu Seleman Ally

18. James Kabalo Mapalala

19. Mary Oswald Mpangala

20. Mwaka Lameck Mgimwa

21. Nancy S. Mrikaria

22. Nakazael Lukio Tenga

23. Fahmi Nasoro Dovutwa

24.Costantine Akitanda

25. Mary Moses Daudi

26. Magdalena Likwina

27. John Dustan Lifa Chipaka

28. Rashid Mohamed Ligania Rai

Tanzania Zanzibar (14)

1. Ally Omar Juma

2. Vuai Ali Vuai

3. Mwanaidi Othman Twahir

4. Jamila Abeid Saleh

5. Mwanamrisho Juma Ahmed

6. Juma Hamis Faki

7. Tatu Mabrouk Haji

8. Fat –Hiya Zahran Salum

9. Hussein Juma

10. Zeudi Mvano Abdullahi

11. Juma Ally Khatibu

12. Haji Ambar Khamis

13. Khadija Abdallah Ahmed

14. Rashid Yussuf Mchenga

Taasisi za Elimu- (Wajumbe 20)

Tanzania Bara

1. Dk Suzan Kolimba

2.Profesa Esther Mwaikambo

3. Dk Natujwa Mvungi

4. Profesa Romuald Haule

5. Dk Domitila A.R. Bashemera

6. Dk Jasmine Tiisekwa

7. Profesa Bernadeta Kilian

8. Teddy Ladislaus Patrick

9. Dk Francis Michael

10. Profesa Remmy J. Assey

11. Dk Tulia Ackson

12.Dk Ave Maria Semakafu

13. Hamza Mustafa Njozi

Tanzania Zanzibar (7)

1. Makame Omar Makame

2. Fatma Hamid Saleh

3. Dk Aley Soud Nassor

4. Layla Ali Salum

5. Dk Mwinyi Talib Haji

6. Zeyana Mohamed Haji

7. Ali Ahmed Uki

Watu Wenye Ulemavu- (Wajumbe 20)

Tanzania Bara (13)

1. Zuhura Musa Lusonge

2. Frederick Msigala

3. Amon Anastaz Mpanju

4. Bure Zahran

5. Edith Aron Dosha

6. Vincent Venance Mzena

7. Shida Salum Mohamed

8. Dk Henry Nyamubi.

9. Elias Msiba Masamaki

10. Faustina Jonathan Urassa

11. Doroth Stephano Malelela

12. John Josephat Ndumbaro

13. Ernest Njama Kimaya

Tanzania Zanzibar (7)

1. Haidar Hashim Madeweyya

2. Alli Omar Makame

3. Adil Mohammed Ali

4. Mwandawa Khamis Mohammed

5. Salim Abdalla Salim

6. Salma Haji Saadat

7. Mwantatu Mbarak Khamis

Vyama vya Wafanyakazi(Wajumbe19)

Tanzania Bara(13)

1. Honorata Chitanda

2. Dk Angelika Semike

3. Ezekiah Tom Oluoch

4. Adelgunda Michael Mgaya

5. Dotto M. Biteko

6. Mary Gaspar Makondo

7. Halfani Shabani Muhogo

8. Yusufu Omari Singo

9. Joyce Mwasha

10. Amina Mweta

11. Mbaraka Hussein Igangula

12. Aina Shadrack Massawe

13. Lucas Charles Malunde

Tanzania Zanzibar (6)

1. Khamis Mwinyi Mohamed

2. Jina Hassan Silima

3. Makame Launi Makame

4. Asmahany Juma Ali

5. Mwatoum Khamis Othman

6. Rihi Haji Ali

Vyama Vinavyowakilisha Wafugaji-(Wajumbe 10)

Tanzania Bara(7)

1. William Tate Olenasha

2. Makeresia Pawa

3. Mabagda Gesura Mwataghu

4. Doreen Maro

5. Magret Nyaga

6. Hamis Mnondwa

7. Ester Milimba Juma

Tanzania Zanzibar (3)

1. Said Abdalla Bakari

2. Mashavu Yahya

3. Zubeir Sufiani Mkanga

Vyama Vinavyowakilisha Wavuvi –(Wajumbe 10)

Tanzania Bara (7)

1. Hawa A. Mchafu

2. Rebecca Masato

3. Thomas Juma Minyaro

4. Timtoza Bagambise

5. Tedy Malulu

6. Rebecca Bugingo

7. Omary S. Husseni

Tanzania Zanzibar (3)

1. Waziri Rajab

2. Issa Ameir Suleiman

3. Mohamed Abdallah Ahmed

Vyama vya Wakulima-(Wajumbe 20)

Tanzania Bara (13)

1. Agatha Harun Senyagwa

2. Veronica Sophu

3. Shaban Suleman Muyombo

4. Catherine Gabriel Sisuti

5. Hamisi Hassani Dambaya

6. Suzy Samson Laizer

7. Dk Maselle Zingura Maziku

8. Abdallah Mashausi

9. Hadijah Milawo Kondo

10. Rehema Madusa

11. Reuben R. Matango

12. Happy Suma

13. Zainab Bakari Dihenga

Tanzania Zanzibar (7)

1. Saleh Moh’d Saleh

2. Biubwa Yahya Othman

3. Khamis Mohammed Salum

4. Khadija Nassor Abdi

5. Fatma Haji Khamis

6. Asha Makungu Othman

7. Asya Filfil Thani

Watu Wenye Malengo Yanayofanana – (Wajumbe 20)

Tanzania Bara (14)

1. Dk Christina Mnzava

2. Paulo Christian Makonda

3. Jesca Msambatavangu

4. Julius Mtatiro

5. Katherin Saruni

6. Abdallah Majura Bulembo

7. Hemedi Abdallah Panzi

8. Dk Zainab Amir Gama

9. Hassan Mohamed Wakasuvi

10. Paulynus Raymond Mtendah

11. Almasi Athuman Maige

12. Pamela Simon Massay

13. Kajubi Diocres Mukajangwa

14. Kadari Singo

Tanzania Zanzibar (6)

1. Yussuf Omar Chunda

2. Fatma Mussa Juma

3. Profesa Abdul Sheriff

4. Amina Abdulkadir Ali

5. Shaka Hamdu Shaka

6. Rehema Said Shamte