Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kaya 130 za Tasaf zapata ajira ya muda Sengerema

Baadhi ya walengwa wa Tasaf Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza wakifanya matengezo ya barabara ya Beipoa Makonge yenye urefu wa kilomita 2.8 kwa kutumia jembe la mkono. Picha Daniel Makaka

Muktasari:

Kaya 130 za walengwa wa Tasaf Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza zimeanza  kunufaika na ajira za muda zitakazo waongezea kipato cha Sh3, 000 kwa siku.

Sengerema. Mpango wa kunusuru kaya masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) umeanza matengezo ya barabara ya Beipoa Makonge iliyopo Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza yenye urefu wa kiliometa 2.8 utakaogharimu Sh64.9 milioni

Matengenezo ya barabara hiyo iliyopo Kata ya Nyatukala yanafanywa na walengwa wa Tasaf wilayani humo wenye miaka kati ya 18 hadi 60 ikiwa ni kutekeleza mradi wa ajira za muda kwa walengwa wake 130 watakaolipwa Sh3, 000 kwa siku.

Akizungumza leo Ijumaa Aprili 14, 2023 wakati wa matengenezo ya barabara hiyo, Mratibu  wa Tasaf Wilaya ya Sengerema, Malisa Nduga amesema mradi huo ni sehemu ya walengwa kujiongezea kipato ambapo watu wanaotakiwa kufanya kazi hizo ni wale wanaotoka kwenye kaya maskini pekee.

Malisa amesema matengezeo ya barabara hiyo yanatarajiwa kukamilika Mei, 30 mwaka huu ili wananchi waweze kuitumia.

“Kumalizika kwa matengenezo ya barabara hiyo kutafungua fursa za kiuchumi kwa wananchi kupitisha mazao yao kupeleka sokoni bila buguza yoyote tofauti na sasa wanalazimika kutoka Kijiji cha Butonga kwenda sokoni mjini Sengerema  wanatumia kilomita sita kuzungukia barabara ya lami,” amesema Malisa 

Mmoja wa wanufaika wa Tasaf wilayani humo, Cesilia Bwiti amesema licha ya kunufaika  kwa kujiongezea kipato kwa kutengeneza barabara hiyo kwa jembe la mkono, kumalizika kwa barabara hiyo  kutafungua fursa ya biashara kwa wananchi wa maeneo  hayo wanaojihusisha na masuala ya kilimo.

“Tunashukuru Serikali kwa kutuona na kutupatia mradi wa kutuongezea kipato. Tunaufanya kwa ufanisi mkubwa,”amesema Bwiti

Kwa upande wake muwakilishi wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) wilayani humo, Fraza Simoni amesema wamepitia barabara yote na kutoa ushauri  juu ya matengenezo yake lengo ni kuhakikisha matengezo hayo yanafanyika kwa ubora unaotakiwa.