Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kero ya wafanyabiashara Zanzibar kutozwa kodi mara mbili yaondolewa

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba akiwasilisha bungeni Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/2024, jijini Dodoma Juni 15, 2023. Picha na Edwin Mjwahuzi

Muktasari:

  • Serikali yasema hoja nne kati ya nane ambazo ni kero za Muungano zimepatiwa ufumbuzi ikiwemo ya wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili.

Dar es Salaam. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema Serikali imezipatia ufumbuzi hoja nne za Muungano ikiwemo ya malalamiko ya wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili.

Dk Nchemba amezitaja kodi hizo ni pamoja na Kodi ya mapato kadri unavyopata  na kodi ya zuio mkataba wa mkopo wa fedha za mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Karume (Terminal III).

"Pia ongezeko la gharama za umeme kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwenda Shirika la Umeme la Zanzibar (Zeco)," ameeleza Dk Mwigulu

Waziri huyo ameeleza hayo leo Alhamisi Juni 15, 2023 wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka 2022/23 akisisitiza Serikali inatambua Muungano ni Tunu ya Taifa letu na ndio utambulisho Tanzania duniani.

"Hivyo ni jukumu letu sote kuulinda, kuudumisha na kuuenzi.Katika kuendelea kudumisha Muungano, Serikali imekuwa ikifanya vikao mbalimbali kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa hoja za Muungano,"amesema.

Ameongeza kuwa katika mwaka 2022/23, Serikali ilijadili hoja nane za Muungano ambapo nne zilipatiwa ufumbuzi na kuondolewa katika orodha ya hoja za Muungano.